1 Wafalme Chapter 13 SWHULB Bible Verse Images

1 Wafalme 13 Bible Verse Pictures. Choose from a large collection of inspirational, motivational and encouraging Bible verses with pictures of nature. Download and share 1 Wafalme 13 inspirational Bible verse images. Bible verse pictures were created based on verses from the Swahili Unlocked Literal Bible (SWHULB). The Holy Bible in the Swahili language, Unlocked Literal Bible version.

Copyright © 2019 Door43 World Missions Community
Language: Kiswahili (Swahili)
Translation by: Door43 World Missions Community

Contributors: Alfred Danjuma, Bariki Malisa, Christina Abraham Kileo, Cloud Roman, Daniel Marura Chacha, Dina Mast, Dina Roman, Donald Shadarck Dutuyi, Emmanuel Masanja Mbaaga, Emmanuel Nyamalya, Erasmus Peter Malelo, Ev. Lazaro Chalomhola, Ezekiel Manala, Fred, Gabriel Gidale Merus, Gabriel Lwitakubi Mazige, James Makula, James Semnkai, Jeremiah Masasi, Jesse Katabi Masolwa, John Ojasi, Joyce Gilbert Masasi, Karen Riecks, Kazwanomo, Kennedy, Ker, Lameck Yakobo Tobotobo, Laurent Petro Malelo, Lazarus David Chalomhola, Makene Mafwele, Marco Luma Mahushi, Mathew Nkusa, Mathias William, Mr. James Semnkai .It., Musa Isaya Majama, Musa Luzali, Pastor John Kerim, Pastor Jordan, Philipo Mussa Kanwelle, Raphael Musa, Rev. Charles Mabisa, Rev. Yohana Batano, Robert Ndalahwa, Sadiki Kulwa, Samson Nungwana, Thobias Kazwanomo, Yohana Dutuyi, Yohana Magera, Zelote Loilang'akaki Lukumay, Rev. Erasmus Peter Malelo, Ev. Mathew Kazimoto, Rev. Dr. David Magoke, Rev. Elias Ndema, Rev. Alex Nyuri, Rev. Gungutu Elias, Rev. Lameck Tobotobo, Rev. Catherin D. Matia, Rev. Yohana S Dutuyi, Rev. Donald Dutuyi, GS. Andrew Gewe, Ev. Ezekiel Daudi, Rev. John Ndaluka, Ev. Moses Malugu, Rev. Moses Eliakim Ndege, Past. Isack A. Gomugo, Past. Mathias William, Rev. Yekonia M. Koko, Rev. Elisande Mhanga, Ev. James A. Makula.

This translation is made available to you under the terms of the Creative Commons Attribution Share-Alike license 4.0.

You have permission to share and redistribute this Bible translation in any format and to make reasonable revisions and adaptations of this translation, provided that:

  • You include the above copyright and source information.
  • If you make any changes to the text, you must indicate that you did so in a way that makes it clear that the original licensor is not necessarily endorsing your changes.
  • If you redistribute this text, you must distribute your contributions under the same license as the original.

Credits: In addition, we would like to give very special thanks to eBible.org for making Swahili Unlocked Literal Bible available in MySQL format.


1 Wafalme 13:1 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mtu wa Mungu alikuja tokea Yuda kwa neno la BWANA kule Betheli. Naye Yeroboamu alikuwa amesimama karibu na madhabahu ili kufukiza uvumba.

1 Wafalme 13:2 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akalia kinyume na zile madhabahu kwa neno la BWANA: “Ee madhabahu, madhabahu” hivi ndivyo asemavyo BWANA, 'Tazama, mwana aitwaye Yosia atazaliwa katika familia ya Daudi, na juu yenu atawachinja makuhani ambao sasa wanafukiza uvumba mahali hapa pa juu kwa ajili yako. Juu yako watachoma mifupa ya watu.'”

1 Wafalme 13:3 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha mtu wa Mungu akatoa ishara siku hiyohiyo, akisema, “Hii ndiyo isharaya kwamba BWANA amesema: 'Tazama, madhabahu zitavuunjika, na majivu yaliyo juu yatamwagika.”

1 Wafalme 13:4 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Naye mfalme aliposikia kile mtu wa Mungu alichosema, kwamba amelia kinyume cha zile madhabahu kule Betheli, Yeroboamu akanyosha mkono wake kutoka madhabahuni, akisema, “mkamateni.” Ndipo ule mkono aliokuwa ameunyosha dhidi ya mtu wa Mungu ukakauka, kiasi kwamba hakuweza kuurudisha mwenyewe.

1 Wafalme 13:5 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Na ile madhabahu ikavunjika vipande vipande, na yale majivu yakamwagika kutoka madhabahuni, kama ilivyokuwa imefafanuliwa kuwa ndiyo ishara ya kwamba mtu wa Mungu alikuwa amepewa kwa neno la BWANA.

1 Wafalme 13:6 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mfalme Yeroboamu akajibu akimwambia mtu wa Mungu, “Msihi BWANA, Mungu wako akupe neema ili uniombee, ili kwamba mkono wangu urejee kwangu tena.” Kwa hiyo mtu wa Mungu akamwomba BWANA, na mkono wa mfalme ukarejea katika hali yake tena, na ukawa kama ulivyokuwa mwanzoni.

1 Wafalme 13:7 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yule mfalme akamwambia mtu wa Mungu, “twende nyumbani kwangu upate chakula, nami nitakupa zawadi.”

1 Wafalme 13:8 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yule mtu wa Mungu akamwambia mfalme, “Hata kama utanipa nusu ya miliki yako. staende na wewe, wala sitakula au kunywa maji mahali hapa,

1 Wafalme 13:9 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
kwa sababu BWANA ameniamuru kwa neno lake, 'hutakula mkate wala kunywa maji, wala kurudi kwa njia ulioijia.'”

1 Wafalme 13:10 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa hiyo mtu wa Mungu akaondoka na hakurudi nyumbani kwa njia aliyokuja nayo huko Betheli.

1 Wafalme 13:11 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Sasa kulikuwa na nabii mwingine mzee aliyekuwa akiishi Betheli, na mmoja wa wana wake akaja kumwambia mambo yote ambayo mtu wa Mungu amefanya siku hiyo kule Betheli. Wana wake wakamwambia pia maneno ambayo Yule mtu wa Mungu alimwambia mfalme.

1 Wafalme 13:12 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Baba yao akawaambia, “Alienda kwa njia gani?” Wale wanawe walikuwa wamemwona yule mtu wa Mungu kutoka Yuda njia aliyotumia kurudi.

1 Wafalme 13:13 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa hiyo akawaambia wanawe, “Nitandikeni punda.” Kwa hiyo wakamtandikia punda naye akampanda.

1 Wafalme 13:14 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yule nabii mzee akamfuata yule mtu wa Mungu na akamkuta amekaa chini ya mti wa mwaloni; akamwambia, “Je, wewe ndiye mtu wa Mungu aliyetoka Yuda?” Naye akamjibu, “Mimi ndiye.”

1 Wafalme 13:15 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha yule nabii mzee akamwambia, “twende nyumbani kwangu ukale chakula.”

1 Wafalme 13:16 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yule mtu wa Mungu akamjibu, “Siwezi kurudi na wewe wala kuingia ndani na wewe, tena sitakula chakula wala kunywa maji pamoja na wewe mahali hapa,

1 Wafalme 13:17 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
kwa sababu niliamuriwa hivyo kwa neno la BWANA, 'Hautakula chakula wala kunywa maji kule, wala kurudi kwa njia utakayokuja nayo.'”

1 Wafalme 13:18 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa hiyo yule nabii mzee akamwambia, “Mimi pia ni nabii kama ulivyo, na malaika amesema na mimi neno la BWANA, akisema, 'Mrudishe aje na wewe katika nyumba yako, ili aweze kula chakula na kunywa maji.'” Lakini alikuwa anamdanganya mtu wa Mungu.

1 Wafalme 13:19 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa hiyo yule mtu wa Mungu akarudi pamoja na yule nabii mzee na akala chakula nyumbani kwake na akanywa maji.

1 Wafalme 13:20 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Walipokuwa wamekaa mezani, neno la BWANA likamjia yule nabii aliyemrudisha,

1 Wafalme 13:21 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
naye akalia kwa mtu wa Mungu aliyetoka Yuda, akisema “BWANA anasema, 'Kwa kuwa umeshindwa kutii nenola BWANA na umeshindwa kuishika amri ya BWANA ambayo Mungu wako alikupa,

1 Wafalme 13:22 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
bali umerudi na umekula chakula na kunywa maji mahali ambapo BWANA alikwambia usile chakula wala kunywa maji, basi mwili wako hautazikwa kwenye makaburi ya baba zako.'”

1 Wafalme 13:23 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Baada ya kula chakula na kunywa maji, Yule nabii akatandika punda wa mtu wa Mungu, yule mtu aliyerudi naye.

1 Wafalme 13:24 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Baada ya mtu wa Mungu kuondoka, akakutana na simba njiani na kumwua barabarani, na mwili wake uliachwa barabarani. Na yule punda akasimama pembeni yake, na yule simba naye akasimama pembeni ya ule mwili.

1 Wafalme 13:25 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Watu walipopita na kuuona ule mwili umeachwa barabarani, na yule simba akisimama karibu na ule mwili, walikuja wakaeleza habari hiyo mjini kule ambako yule nabii mzee aliishi.

1 Wafalme 13:26 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yule nabii aliyemrudisha toka njiani aliposikia, akasema, “Yeye mtu wa Muugu ndiye aliyeshindwa kutii neno la BWANA. Kwa hiyo BWANA alimtoa kwa simba, ambaye amemrarua katika vipande vipande na kumwua, kama vile neno la BWANA lilivyokuwa limemwonya.”

1 Wafalme 13:27 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa hiyo yule nabii mzee akawaamnbia wanawe, akisema, “Tandikeni punda wangu,” nao wakamtandikia.

1 Wafalme 13:28 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akaenda akaukuta mwili umeachwa barabarani, punda na simba wamesimama pembeni ya ule mwili. Yule simba hakuula ule mwili, wala hakumshambulia yule punda.

1 Wafalme 13:29 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yule nabii akauchukua ule mwili wa mtu wa Mungu, akaulaza juu ya punda, na akaurudisha. Akaja kwenye mji wake kuomboleza na kuuzika.

1 Wafalme 13:30 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akaulaza mwili kwenye kaburi lake, nao wakamwombolezea, wakisema, “Aa! ndugu yangu!”

1 Wafalme 13:31 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha baada ya kumzika, yule nabii mzee akawaambia wanawe, akasema, “Nitakapokufa, mtanizika kwenye kaburi ambalo tumemzika mtu wa Mungu. Mtalaza mifupa yangu pembeni mwa mifupa yake.

1 Wafalme 13:32 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa kuwa ule ujumbe uliosemwa na BWANA, dhidi ya madhabahu kule Betheli na dhidi ya nyumba zote za mahali pa juu katika mji wa Samaria, hakika yatatokea.

1 Wafalme 13:33 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Baada ya haya Yeroboamu hakuuacha uovu wake, aliendelea kuchagua makuhani wa kawaida kwa ajili ya mahali pa juu kutoka kwa watu wa kila aina. Yeyote ambaye angeweza kutumika alimtakasa kuwa kuhani.

1 Wafalme 13:34 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Jambo hili likawa dhambi kwenye familia ya Yeroboamu na kusababisha familia yake kuangamizwa na kuondolewa kabisa katika uso wa dunia.
Previous Chapter
« 1 Wafalme 12 (SWHULB)

Available Bible Translations

American Standard Version
1 Kings 13 (ASV) »
King James Version
1 Kings 13 (KJV) »
GOD’S WORD® (GW)
1 Kings 13 (GW) »
World English Bible
1 Kings 13 (WEB) »
Louis Segond 1910
1 Rois 13 (LSG) »
इंडियन रिवाइज्ड वर्जन - हिंदी
1 राजाओं 13 (HINIRV) »
ਭਾਰਤੀ ਸੋਧਿਆ ਹੋਇਆ ਸੰਸਕਰਣ - ਪੰਜਾਬੀ
1 ਰਾਜਿਆਂ 13 (PANIRV) »
ভারতীয় সংশোধিত সংস্করণ - বাংলা
1 ৰাজাৱলী 13 (BENIRV) »
இந்தியன் ரீவைஸ்டு வேர்ஷன் - தமிழ்
1 இராஜாக்கள் 13 (TAMIRV) »
इंडियन रिवाइज्ड वर्जन - मराठी
1 राजे 13 (MARIRV) »
ఇండియన్ రేవిజ్డ్ వెర్షన్ - తెలుగు
1 రాజులు 13 (TELIRV) »
ઇન્ડિયન રિવાયઝ્ડ વર્ઝન - ગુજરાતી
1 રાજાઓ 13 (GUJIRV) »
ಭಾರತೀಯ ಪರಿಷ್ಕೃತ ಆವೃತ್ತಿ - ಕನ್ನಡ
1 ಅರಸುಗಳು 13 (KANIRV) »
الكتاب المقدس باللغة العربية، فان دايك
اَلْمُلُوكِ ٱلْأَوَّلُ 13 (AVD) »
תנ ך עברי מודרני
מלכים א 13 (HEB) »
Bíblia Sagrada Português
1 Reis 13 (BSL) »
Kinh Thánh: Tiếng Việt
1 Các Vua 13 (VIE) »
Reina Valera Antigua
1 Reyes 13 (RVA) »
La Sacra Bibbia
1 Re 13 (RIV) »
圣 经 简体中文和合本
列 王 记 上 13 (CUVS) »
聖 經 繁體中文和合本
列 王 紀 上 13 (CUVT) »
Svenska Bibeln 1917
1 Kungaboken 13 (SV1917) »
Библия на русском
3 Царств 13 (RUSV) »
Українська Біблія
1 царів 13 (UKR) »
Szent Biblia - Magyar
1 Királyok 13 (KAR) »
Българска Библия
3 Царе 13 (BULG) »
Kitaabka Quduuska Ah
Boqorradii Kowaad 13 (SOM) »
De Heilige Schrift
1 Koningen 13 (NLD) »

1 Wafalme (SWHULB) Chapter Selection

SWHULB Book Selection List