Danieli Chapter 2 SWHULB Bible Verse Images

Danieli 2 Bible Verse Pictures. Choose from a large collection of inspirational, motivational and encouraging Bible verses with pictures of nature. Download and share Danieli 2 inspirational Bible verse images. Bible verse pictures were created based on verses from the Swahili Unlocked Literal Bible (SWHULB). The Holy Bible in the Swahili language, Unlocked Literal Bible version.

Copyright © 2019 Door43 World Missions Community
Language: Kiswahili (Swahili)
Translation by: Door43 World Missions Community

Contributors: Alfred Danjuma, Bariki Malisa, Christina Abraham Kileo, Cloud Roman, Daniel Marura Chacha, Dina Mast, Dina Roman, Donald Shadarck Dutuyi, Emmanuel Masanja Mbaaga, Emmanuel Nyamalya, Erasmus Peter Malelo, Ev. Lazaro Chalomhola, Ezekiel Manala, Fred, Gabriel Gidale Merus, Gabriel Lwitakubi Mazige, James Makula, James Semnkai, Jeremiah Masasi, Jesse Katabi Masolwa, John Ojasi, Joyce Gilbert Masasi, Karen Riecks, Kazwanomo, Kennedy, Ker, Lameck Yakobo Tobotobo, Laurent Petro Malelo, Lazarus David Chalomhola, Makene Mafwele, Marco Luma Mahushi, Mathew Nkusa, Mathias William, Mr. James Semnkai .It., Musa Isaya Majama, Musa Luzali, Pastor John Kerim, Pastor Jordan, Philipo Mussa Kanwelle, Raphael Musa, Rev. Charles Mabisa, Rev. Yohana Batano, Robert Ndalahwa, Sadiki Kulwa, Samson Nungwana, Thobias Kazwanomo, Yohana Dutuyi, Yohana Magera, Zelote Loilang'akaki Lukumay, Rev. Erasmus Peter Malelo, Ev. Mathew Kazimoto, Rev. Dr. David Magoke, Rev. Elias Ndema, Rev. Alex Nyuri, Rev. Gungutu Elias, Rev. Lameck Tobotobo, Rev. Catherin D. Matia, Rev. Yohana S Dutuyi, Rev. Donald Dutuyi, GS. Andrew Gewe, Ev. Ezekiel Daudi, Rev. John Ndaluka, Ev. Moses Malugu, Rev. Moses Eliakim Ndege, Past. Isack A. Gomugo, Past. Mathias William, Rev. Yekonia M. Koko, Rev. Elisande Mhanga, Ev. James A. Makula.

This translation is made available to you under the terms of the Creative Commons Attribution Share-Alike license 4.0.

You have permission to share and redistribute this Bible translation in any format and to make reasonable revisions and adaptations of this translation, provided that:

  • You include the above copyright and source information.
  • If you make any changes to the text, you must indicate that you did so in a way that makes it clear that the original licensor is not necessarily endorsing your changes.
  • If you redistribute this text, you must distribute your contributions under the same license as the original.

Credits: In addition, we would like to give very special thanks to eBible.org for making Swahili Unlocked Literal Bible available in MySQL format.


Danieli 2:1 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Katika mwaka wa pili wa utawala wa Nebukadneza, alikuwa na ndoto. Akili yake ilisumbuka, na hakuweza kulala.

Danieli 2:2 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo mfalme alipowaita waganga na wale wenye kuongea na wafu. Lakini pia aliwaita wachawi na watu wenye hekima. Aliwataka wamwambie juu ya ndoto zake. Basi walikuja na kusimama mbele za mfalme.

Danieli 2:3 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mfalme akawambia, “Nilikuwa na ndoto, na akili yangu ina mashaka nataka kujua ndoto hiyo nini maana yake.”

Danieli 2:4 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha watu wenye hekima wakamwambia mfalme katika Kiaramaiki, “ Mfalme, aishi milele! Twambie sisi ndoto, watumishi wako, nasi tutaifunua maana yake.”

Danieli 2:5 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mfalme akawajibu watu wenye hekima, “ Jambo hili limeshamalizika. Kama hamtaweza kuiweka wazi ndoto kwangu na kuitafsiri, miili yenu itakatwa vipande vipande na nyumba zenu zitafanywa kuwa vichuguu vya uchafu.

Danieli 2:6 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini kama mtaniambia ndoto na maana yake, mtapokea zawadi kutoka kwangu, thawabu, na heshima kubwa. Basi niambie ndoto na maana yake.”

Danieli 2:7 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakamjibu tena na kusema, “Mfalme na atuambie, watumishi wake, ndoto nasi tukwambia maana yake.”

Danieli 2:8 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mfalme akawajibu, “ Ninajua kwa hakika mnahitaji muda zaidi kwasababu mmeona maamuzi yangu ni magumu kuhusu jambo hili.

Danieli 2:9 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini kama hamtaweza kuniambia ndoto, kuna sentensi moja tu kwa ajili yenu. Mmeamua kuandaa uongo na maneno ya kudanganya ambayo mmekubaliana kwa pamoja kuniambia mpaka pale nitakapobadili akili zangu. Basi, niambieni ndoto, na kisha nitajua kuwa mnaweza kuitafsiri kwa ajili yangu.”

Danieli 2:10 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Watu wenye hekima wakamjibu mfalme, “ Hakuna mtu katika dunia anayeweza kutimiza matakwa ya mfalme. Hakuna mfalme yoyote mkuu na mwenye nguvu ambaye alishataka jambo kama hilo kutoka kwa wachawi, wala wenye kuongea na wafu, wala mwenye hekima.

Danieli 2:11 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kile anachokitaka mfalme ni kigumu, na hakuna yeyote awezaye kumwambia mfalme isipokuwa miungu, ambayo haishi miongoni mwa watu.”

Danieli 2:12 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Jambo hili lilimfanya mfalme akasirike na kughadhabika sana, na alitoa amri kuwaangamiza wale wote waliojulikana kuwa ni wenye hekima zao katika Babeli.

Danieli 2:13 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hivyo, amri ilitoka kwamba wale wote waliojulikana kwa hekima yao ni lazima wauawe. Na kwa sababu ya amri hii, walimtafuta Daniel na rafiki zake ili kwamba wauawe.

Danieli 2:14 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo Daniel alipomjibu kwa busara na umakini, Arioki, kamanda wa walinzi wa mfalme, ambaye alikuwa amekuja kuwaua wale wote waliojulikana kuwa na hekima katika Babeli.

Danieli 2:15 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Danieli alimwuliza kamanda wa mfalme, “ Kwanini amri ya mfalme ni ya haraka hivyo?” Hivyo, Arioki akamwambia Danieli kile kilichotokea.

Danieli 2:16 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo Danieli aliingia ndani na akaomba ahadi ya muda wa kuonana na mfalme ili kwamba aweze kuwasilisha tafsiri kwa mfalme.

Danieli 2:17 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha Danieli aliingia ndani ya nyumba na aliwaelezea Hanania, Mishaeli, na Azaria, kile kilichotokea.

Danieli 2:18 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Aliwasihi kutafuta rehema kutoka kwa Mungu wa mbinguni kuhusiana na siri hii ili kwamba yeye na wao wasije wakauawa pamoja na watu wengine waliosalia waliojulikana kuwa na hekima katika Babeli.

Danieli 2:19 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Usiku ule siri ilifunuliwa kwa Danieli katika maono. Kisha Danieli akamtukuza Mungu wa mbinguni

Danieli 2:20 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
na kusema, “Litukuzwa jina la Mungu milele na milele; kwa kuwa hekima na nguvu ni zake.

Danieli 2:21 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Anabadili wakati na majira; anaondoa wafalme na kuweka wafalme katika viti vyao vya enzi. Anawapa hekima wenye hekima na ufahamu kwa wenye weledi.

Danieli 2:22 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hufunua vitu vya chini na vilifichika kwa sababu anajua kile kilicho gizani, naye anaishi pamoja na mwanga.

Danieli 2:23 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mungu wa baba zetu, ninakushukuru na kukutukuza wewe kwa ajili ya hekima na nguvu uliyonipa. Sasa umeyafanya yawe wazi kwetu yale tuliyokuomba; umetujulisha mambo yamhusuyo mfalme.”

Danieli 2:24 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo Danieli alienda kumwona Arioki ( yule ambaye mfalme alimchagua kuua kila mtu aliyekuwa na hekima katika Babeli). Alimwendea na kumwambia, “Usiwauwe watu wenye hekima katika Babeli. Nipeleke kwa mfalme na nitamwonesha mfalme tafsiri ya ndoto yake.”

Danieli 2:25 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha Arioki kwa haraka alimleta Danieli mbele za mfalme na kusema, “ Nimempata miongoni wa watu wa mateka wa Yuda mtu ambaye atafunua maana ya ndoto ya mfalme.”

Danieli 2:26 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mfalme akamwambia Danieli (ambaye alikuwa akiitwa Beliteshaza), “Je unaweza kunimbia ndoto niliyoiona na maana yake?”

Danieli 2:27 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Danieli alimjibu mfalme na kusema, “Siri ambayo mfalme ameiomba haiwezi kufunuliwa na watu wenye hekima, wala wale wenye kuongea na wafu, wala wachawi, na wala wataalamu wa nyota.

Danieli 2:28 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Isipokuwa kuna Mungu ambaye anaishi mbinguni, ambaye hufunua siri, na amekwisha kukujulisha wewe, mfalme Nebukadneza, kile kitakachotokea katika siku zijazo. Hizi ndizo Ndoto na maono ya akili zako uliyoyaona wakati ulipokuwa umelala kitandani mwako.

Danieli 2:29 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Na kwako Wewe, mfalme, mawazo yako kitandani mwako yalikuwa ni juu ya mambo yajayo, na yule afichuaye siri ameifanya ijulikane kwako kuhusu kile kilicho karibu kutokea.

Danieli 2:30 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Na kuhusu mimi, siri hii haikufunuliwa kwangu kwa sababu ya hekima yoyote niliyo nayo zaidi ya mtu yoyote anayeishi. Siri hii imefunliwa kwangu ili kwamba wewe, mfalme, uweze kufahamu maana, na ili kwamba ujuwe mawazo yaliyo ndani mwako.

Danieli 2:31 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mfalme, uliangalia juu na ukaona sanamu kubwa. Sanamu hii ambayo ilikuwa yenye nguvu na yenye kung'aa, ilisimama mbele yako. Mng'ao wake ulikuwa unatisha.

Danieli 2:32 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kichwa cha sanamu kilikuwa kimetengenezwa kwa dhahabu safi. Matiti yake na mikono ilikuwa ya fedha. Sehemu ya katikati na mapaja yake yalikuwa yametengenezwa kwa shaba,

Danieli 2:33 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
na miguu yake ilikuwa imetengenezwa kwa chuma. Miguu yake ilikuwa ilitengenezwa kwa sehemu chuma na sehemu kwa udongo.

Danieli 2:34 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ulitazama juu, na jiwe lilikuwa limechongwa, ingawa si kwa mikono ya wanadamu, na liliipiga sanamu katika miguu yake ya chuma na udongo, na ponda ponda.

Danieli 2:35 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha chuma, udongo, fedha, na dhahabu zilivunjwa katika vipande vipande kwa wakati mmoja na yakawa kama makapi yaliyo katika sakafu za kupuria kipindi cha kiangazi. Upepo huyapeperushia mbali na hakuna alama inayoachwa. Lakini jiwe lililoipiga sanammu likawa mlima mkubwa na kuijaza dunia yote.

Danieli 2:36 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hii ndiyo ilikuwa ndotoyako. Na sasa tutamwambia mfalme maana yake.

Danieli 2:37 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wewe, mfalme, ni mfalme wa wafalme kwa wale ambao Mungu wa mbinguni amekupa ufalme, nguvu, uweza na heshima.

Danieli 2:38 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Amevitia mkononi mwako sehemu ambazo binadamu huishi. Amekupa wanyama wa mwituni na ndege wa angani katika mkono wako, na amekufanya wewe utawale juu yao wote. Wewe u kichwa cha dhahabu cha sanamu.

Danieli 2:39 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Baada yako, ufalme mwingine utainuka ambao ni mdogo kwako, na hata ufalme wa tatu wa shaba utatawala juu ya dunia yote.

Danieli 2:40 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kutakuwa na ufalme wa tatu, wenye nguvu kama chuma, kwa kuwa chuma huvunja vipande vipande vitu vingine na kuponda ponda kila kitu. Itaviharibu vitu hivi vyote na kuvisaga.

Danieli 2:41 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kama vile ulivyoona, miguu na vidole vilikuwa kwa sehemu vimetengenezwa kwa udongo na kwa sehemu vimefanywa kwa chuma, hivyo utakuwa ni ufalme uliogawanyika; baadhi ya nguvu za chuma zitakuwa ndani yake, kama tu ulivyoona kuwa chuma kimechanganyikana na udongo laini.

Danieli 2:42 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kama vile vidole vya miguuni vilivyokuwa kwa sehemu vimetengenezwa kwa chuma na kwa sehemu vimetengenezwa kwa udongo, ndivyo ufalme utakuwa kwa sehemu una nguvu na kwa sehemu utakuwa dhaifu.

Danieli 2:43 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kama ulivyoona chuma kimechanganywa na udongo laini, na hivyo na watu watakuwa wamechanganyikana; hawakaa kwa pamoja, kama vile chuma kisivyoweza kushikamana na udongo

Danieli 2:44 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Katika siku za wafalme hao, Mungu wa mbinguni ataanzisha ufalme ambao hautaweza kuangushwa, wala kushindwa na watu wengine. Utazivunja falme zingine vipande vipande na kuzikomesha zote, nao utadumu milele.

Danieli 2:45 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kama tu ulivyoona, jiwe lilichongwa kutoka katika mlima, lakini si kwa mikono ya wanadamu. Lilivunja vunja chuma, shaba, udongo, fedha, na dhahabu katika vipande vipande. Mungu mkuu amekujulisha wewe, mfalme, kile kitakachotokea baada ya haya. Ndoto ni ya kweli na tafsiri yake ni ya kuaminika.

Danieli 2:46 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mfalme Nebukadneza alianguka kifudifudi mbele ya Daniel na alimweshimu; aliamuru kwamba sadaka zitolewe na manukato yatolewe kwake.

Danieli 2:47 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mfalme alimwambia Danieli, “ Hakika Mungu wako ni Mungu wa miungu, Bwana wa wafalme, na ambaye hufunua mafumbo, kwa kuwa umekuwa ukiweza kufumbua mafumbo haya.”

Danieli 2:48 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo mfalme alimfanya Danieli kuwa wa kuheshiwa sana na alimpa zawadi nyingi nzuri. Alimfanya kuwa mtawala juu ya jimbo lote la Babeli. Danieli akawa liwali mkuu juu watu wenye hekima wa Babeli.

Danieli 2:49 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Danieli alipeleka ombi kwa mfalme, na mfalme aliwateua Shadraka, Meshaki na Abedinego kuwa watawala juu ya jimbo la Babeli. Lakini Danieli alisalia katika ikulu ya mfalme.
Previous Chapter
« Danieli 1 (SWHULB)
Next Chapter
Danieli 3 (SWHULB) »

Available Bible Translations

American Standard Version
Daniel 2 (ASV) »
King James Version
Daniel 2 (KJV) »
GOD’S WORD® (GW)
Daniel 2 (GW) »
Berean Bible
Daniel 2 (BSB) »
World English Bible
Daniel 2 (WEB) »
Louis Segond 1910
Daniel 2 (LSG) »
Luther Bibel 1912
Daniel 2 (LUTH1912) »
इंडियन रिवाइज्ड वर्जन - हिंदी
दानिय्येल 2 (HINIRV) »
ਭਾਰਤੀ ਸੋਧਿਆ ਹੋਇਆ ਸੰਸਕਰਣ - ਪੰਜਾਬੀ
ਦਾਨੀਏਲ 2 (PANIRV) »
ভারতীয় সংশোধিত সংস্করণ - বাংলা
দানিয়েল 2 (BENIRV) »
இந்தியன் ரீவைஸ்டு வேர்ஷன் - தமிழ்
தானியேல் 2 (TAMIRV) »
इंडियन रिवाइज्ड वर्जन - मराठी
दानिएल 2 (MARIRV) »
ఇండియన్ రేవిజ్డ్ వెర్షన్ - తెలుగు
దానియేలు 2 (TELIRV) »
ઇન્ડિયન રિવાયઝ્ડ વર્ઝન - ગુજરાતી
દાનિયેલ 2 (GUJIRV) »
ಭಾರತೀಯ ಪರಿಷ್ಕೃತ ಆವೃತ್ತಿ - ಕನ್ನಡ
ದಾನಿಯೇಲನು 2 (KANIRV) »
الكتاب المقدس باللغة العربية، فان دايك
دَانِيآل 2 (AVD) »
תנ ך עברי מודרני
דניאל 2 (HEB) »
Bíblia Sagrada Português
Daniel 2 (BSL) »
Kinh Thánh: Tiếng Việt
Ða-ni-ên 2 (VIE) »
Reina Valera Antigua
Daniel 2 (RVA) »
La Sacra Bibbia
Daniele 2 (RIV) »
圣 经 简体中文和合本
但 以 理 书 2 (CUVS) »
聖 經 繁體中文和合本
但 以 理 書 2 (CUVT) »
Bibla e Shenjtë
Danieli 2 (ALB) »
Svenska Bibeln 1917
Daniel 2 (SV1917) »
Библия на русском
Даниил 2 (RUSV) »
Українська Біблія
Даниїл 2 (UKR) »
Szent Biblia - Magyar
Dániel 2 (KAR) »
Българска Библия
Данаил 2 (BULG) »
Det Norsk Bibel
Daniel 2 (NORSK) »
Kitaabka Quduuska Ah
Daanyeel 2 (SOM) »
De Heilige Schrift
Daniël 2 (NLD) »
Dansk Bibel 1871
Daniel 2 (DA1871) »

Danieli (SWHULB) Chapter Selection

1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12

SWHULB Book Selection List