Yeremia Chapter 29 SWHULB Bible Verse Images

Yeremia 29 Bible Verse Pictures. Choose from a large collection of inspirational, motivational and encouraging Bible verses with pictures of nature. Download and share Yeremia 29 inspirational Bible verse images. Bible verse pictures were created based on verses from the Swahili Unlocked Literal Bible (SWHULB). The Holy Bible in the Swahili language, Unlocked Literal Bible version.

Copyright © 2019 Door43 World Missions Community
Language: Kiswahili (Swahili)
Translation by: Door43 World Missions Community

Contributors: Alfred Danjuma, Bariki Malisa, Christina Abraham Kileo, Cloud Roman, Daniel Marura Chacha, Dina Mast, Dina Roman, Donald Shadarck Dutuyi, Emmanuel Masanja Mbaaga, Emmanuel Nyamalya, Erasmus Peter Malelo, Ev. Lazaro Chalomhola, Ezekiel Manala, Fred, Gabriel Gidale Merus, Gabriel Lwitakubi Mazige, James Makula, James Semnkai, Jeremiah Masasi, Jesse Katabi Masolwa, John Ojasi, Joyce Gilbert Masasi, Karen Riecks, Kazwanomo, Kennedy, Ker, Lameck Yakobo Tobotobo, Laurent Petro Malelo, Lazarus David Chalomhola, Makene Mafwele, Marco Luma Mahushi, Mathew Nkusa, Mathias William, Mr. James Semnkai .It., Musa Isaya Majama, Musa Luzali, Pastor John Kerim, Pastor Jordan, Philipo Mussa Kanwelle, Raphael Musa, Rev. Charles Mabisa, Rev. Yohana Batano, Robert Ndalahwa, Sadiki Kulwa, Samson Nungwana, Thobias Kazwanomo, Yohana Dutuyi, Yohana Magera, Zelote Loilang'akaki Lukumay, Rev. Erasmus Peter Malelo, Ev. Mathew Kazimoto, Rev. Dr. David Magoke, Rev. Elias Ndema, Rev. Alex Nyuri, Rev. Gungutu Elias, Rev. Lameck Tobotobo, Rev. Catherin D. Matia, Rev. Yohana S Dutuyi, Rev. Donald Dutuyi, GS. Andrew Gewe, Ev. Ezekiel Daudi, Rev. John Ndaluka, Ev. Moses Malugu, Rev. Moses Eliakim Ndege, Past. Isack A. Gomugo, Past. Mathias William, Rev. Yekonia M. Koko, Rev. Elisande Mhanga, Ev. James A. Makula.

This translation is made available to you under the terms of the Creative Commons Attribution Share-Alike license 4.0.

You have permission to share and redistribute this Bible translation in any format and to make reasonable revisions and adaptations of this translation, provided that:

  • You include the above copyright and source information.
  • If you make any changes to the text, you must indicate that you did so in a way that makes it clear that the original licensor is not necessarily endorsing your changes.
  • If you redistribute this text, you must distribute your contributions under the same license as the original.

Credits: In addition, we would like to give very special thanks to eBible.org for making Swahili Unlocked Literal Bible available in MySQL format.


Yeremia 29:1 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Haya ni maneno katika waraka ambao Yeremia nabii alituma kutoka Yerusalemu kwa wazee waliosalia miongoni mwa mateka na makuhuni, manabii, na watu wote ambao Nebukadreza aliwapeleka utumwani kutoka Yerusalemu hadi Babeli.

Yeremia 29:2 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hii ilikuwa baada ya Yekonia mfalme, mama yake mfalme, na watumishi wakuu, viongozi wa Yuda na Yerusalemu, na wahunzi walikuwa wamepelekwa mbali na Yerusalemu.

Yeremia 29:3 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Aliutuma waraka huu kwa mkono wa Elasa mwana wa Shafani, Gemaria, mwana wa Hilkia, ambaye Sedekia, mfalme wa Yuda, alikuwa amemtuma kwa Nebukadreza mfalme wa Babeli

Yeremia 29:4 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Waraka ulisema, Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi kwa mateka ambao niliwasababisha kuwa mateka kutoka Yerusalemu hadi Babeli,

Yeremia 29:5 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
'Jengeni nyumba na muishi ndani yake. Pandeni bustani na mle matunda yake.

Yeremia 29:6 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Chukueni wake na mzae wana na mabinti. Kisha Kisha chukueni wake kwa ajili ya wana wenu, na wapatieni waume binti zenu. Wazae wana na mabinti na waongezeke ili msiwe wachache sana.

Yeremia 29:7 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Itafuteni amani ya mji ambako nimewafanya kuwa watumwa, na mkauombee kwangu kwa niaba yake kwa kuwa kutakuwa na amani kwenu kama mji uko katika amani.'

Yeremia 29:8 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa maana Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi, 'Msiwaache manabii ambao wako katikati yenu na wabashiri wenu kuwadanganya, na msizisikilize ndoto ambazo ninyi wenyewe mnaota.

Yeremia 29:9 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa maana wanatabiri uongo kwenu katika jina langu. Mimi sikuwatuma—hili ni tangazo la Yahwe.'

Yeremia 29:10 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa maana Yahwe anasema hivi, 'Babeli atakapokuwa amewatawala kwa muda wa mika sabini, nitawasaidia ninyi na kulitimiza neno langu jema kwa ajili yenu ili kuwarudisha ninyi katika sehemu hii.

Yeremia 29:11 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa maana mimi mwenyewe naijua mipangao niliyonayo kwa ajili yenu—hili ni tangazo la Yahwe—mipango kwa ajili ya amani na siyo kwa ajili ya mabaya, ili kuwapa ninyi tumaini na siku zenu za mwisho.

Yeremia 29:12 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha mtaniita, na kwenda na kuniomba mimi, na nitawasikiliza.

Yeremia 29:13 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa maana mtanitafuta na kunipata, kwa kuwa mtanitafuta kwa moyo wenu wote.

Yeremia 29:14 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha nitapatikana kwenu—hili ni tangazo la Yahwe—na nitawarudisha watu wenu waliofungwa; nitawakusanya kutoka mataifa yote na sehehemu zote ambako nimewatawanya—hili ni tangazo la Yahwe—kwa maana nitawarudisha kutoka sehemu ambako niliwasababisha kuwa mateka.

Yeremia 29:15 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Tangu mliposema kwamba Yahwe ameinua manabii kwa ajili yetu katika Babeli,

Yeremia 29:16 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yahwe anasema hivi kwa mfalme aliyeketi katika kiti cha enzi cha Daudi na watu wote wakaao katika mji huo, ndugu zenu ambao hawakwenda pamoja nanyi utumwani—

Yeremia 29:17 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yahwe wa majeshi anasema hivi, ''Ona, niko karibu kutuma upanga, njaa, na ugonjwa juu yao. Kwa maana nitawafanya kuwa kama tini mbovu ambazo ni mbaya sana hazifai kuliwa.

Yeremia 29:18 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha nitawafuata kwa upanga, njaa, na tauni na kuwafanya kuwa kitu cha kushangaza kwa falme zote juu ya dunia—kitu cha kuogofya, kitu cha kulaaniwa na kuzomewa, na kitu cha aibu miongoni mwa mataifa yote ambako nilimtawanya.

Yeremia 29:19 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hii ni kwa sababu hawakulisikiliza neno langu—hili ni tangazo la Yahwe—ambalo nililituma kwao kupitia watumishi wangu manabii. Niliwatuma tena na tena, lakini hamkusikiliza—hili ni tangazo la Yahwe. '

Yeremia 29:20 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa hiyo ninyi wenyewe sikilizeni neno la Yahwe, ninyi mateka wote ambao amewatuma kutoka Yerusalemu hadi Babeli,

Yeremia 29:21 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
'Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi kuhusu Ahabu mwana wa Kolaya na Sedekia mwana wa Maaseya, watabirio uongo kwenu katika jina langu: Ona, niko karibu kuwaweka katika mkono wa Nebukadreza mfalme wa Babeli. Atawaua mbele ya macho yenu.

Yeremia 29:22 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha laana itatamkwa na wafungwa wote wa Yuda katika Babeli kuhusu watu hawa. Laana itasema: Yahwe awafanye kuwa kama Sedekia na Ahabu, ambao mfalme wa Babeli aliwaoka kwenye moto.

Yeremia 29:23 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hili litatokea kwa sababu ya mambo ya aibu waliyofanya katika Israeli walipofanya uzinzi na wake za majarani zao na kutangaza maneno ya uongo katika jina langu, mambo ambayo sikuwaamuru wayaseme. Kwa maana mimi ndiye nijuaye; mimi ni shahidi—hili ni tangazo la Yahwe.”'

Yeremia 29:24 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kuhusu Shemaya Mnehelami, sema hivi:

Yeremia 29:25 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
'Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kwa sababu ulituma barua kwa jina lako kwa watu wote katika Yerusalemu, kwa Sefania mwana wa Maaseya kuhani, na kwa makuhani wote, na ulisema,

Yeremia 29:26 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
“Yahwe aliwafanya ninyi kuwa makuhani badala ya Yehoyada kuhani, ili muwe wasimamizi wa nyumba ya Yahwe. Ninyi ni viongozi wa watu wote wajitiao wazimu na kujifanya wenyewe manabii. Mtawaweka katika mkatale na minyororo.

Yeremia 29:27 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa hiyo sasa, kwa nini hamkumkemea Yeremia wa Anathothi, ambaye hujifanya mwenyewe nabii juu yenu?

Yeremia 29:28 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa maana ametutumia sisi katika Babeli, 'Itakuwa muda mrefu. Jengeni nyumba na muishi ndani yake, na pandeni busitani na mule matunda yake.””

Yeremia 29:29 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Sefania kuhani akaisoma barua hii mbele ya Yeremia nabii.

Yeremia 29:30 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha neno la Yahwe likaja kwa Yeremia, likisema,

Yeremia 29:31 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
“tuma neno kwa mateka wote na sema, 'Yahwe anasema hivi kuhusu Shemaya Mnehelami: Kwa sababu Shemaya amewatabiria ninyi wakati mimi sikumtuma, na amewaongoza kuamini uongo,

Yeremia 29:32 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
kwa hiyo Yahwe anasema hivi: Angalia, niko karibu kumwadhibu Shemaya Mnehelami na uzao wake. Hapatakuwa na mtu wa kukaa miongoni mwa watu hawa kwa ajili yake. Hataona mema nitakayofanya kwa ajili ya watu wangu—hili ni tangazo la Yahwe—kwa maana ametangaza uasi dhidi ya Yahwe.””
Previous Chapter
« Yeremia 28 (SWHULB)

Available Bible Translations

American Standard Version
Jeremiah 29 (ASV) »
King James Version
Jeremiah 29 (KJV) »
GOD’S WORD® (GW)
Jeremiah 29 (GW) »
World English Bible
Jeremiah 29 (WEB) »
Louis Segond 1910
Jérémie 29 (LSG) »
Luther Bibel 1912
Jeremia 29 (LUTH1912) »
इंडियन रिवाइज्ड वर्जन - हिंदी
यिर्मयाह 29 (HINIRV) »
ਭਾਰਤੀ ਸੋਧਿਆ ਹੋਇਆ ਸੰਸਕਰਣ - ਪੰਜਾਬੀ
ਯਿਰਮਿਯਾਹ 29 (PANIRV) »
ভারতীয় সংশোধিত সংস্করণ - বাংলা
যিৰিমিয়া 29 (BENIRV) »
இந்தியன் ரீவைஸ்டு வேர்ஷன் - தமிழ்
எரேமியா 29 (TAMIRV) »
इंडियन रिवाइज्ड वर्जन - मराठी
यिर्मया 29 (MARIRV) »
ఇండియన్ రేవిజ్డ్ వెర్షన్ - తెలుగు
యిర్మీయా 29 (TELIRV) »
ઇન્ડિયન રિવાયઝ્ડ વર્ઝન - ગુજરાતી
યર્મિયા 29 (GUJIRV) »
ಭಾರತೀಯ ಪರಿಷ್ಕೃತ ಆವೃತ್ತಿ - ಕನ್ನಡ
ಯೆರೆಮೀಯನು 29 (KANIRV) »
الكتاب المقدس باللغة العربية، فان دايك
إِرْمِيَا 29 (AVD) »
תנ ך עברי מודרני
ירמיה 29 (HEB) »
Bíblia Sagrada Português
Jeremias 29 (BSL) »
Kinh Thánh: Tiếng Việt
Giê-rê-mi-a 29 (VIE) »
Reina Valera Antigua
Jeremías 29 (RVA) »
La Sacra Bibbia
Geremia 29 (RIV) »
圣 经 简体中文和合本
耶 利 米 书 29 (CUVS) »
聖 經 繁體中文和合本
耶 利 米 書 29 (CUVT) »
Bibla e Shenjtë
Jeremia 29 (ALB) »
Svenska Bibeln 1917
Jeremia 29 (SV1917) »
Библия на русском
Иеремия 29 (RUSV) »
Українська Біблія
Єремія 29 (UKR) »
Szent Biblia - Magyar
Jeremiás 29 (KAR) »
Българска Библия
Еремия 29 (BULG) »
Det Norsk Bibel
Jeremia 29 (NORSK) »
Kitaabka Quduuska Ah
Yeremyaah 29 (SOM) »
De Heilige Schrift
Jeremia 29 (NLD) »
Dansk Bibel 1871
Jeremias 29 (DA1871) »

Yeremia (SWHULB) Chapter Selection

SWHULB Book Selection List