Marko Chapter 2 SWHULB Bible Verse Images

Marko 2 Bible Verse Pictures. Choose from a large collection of inspirational, motivational and encouraging Bible verses with pictures of nature. Download and share Marko 2 inspirational Bible verse images. Bible verse pictures were created based on verses from the Swahili Unlocked Literal Bible (SWHULB). The Holy Bible in the Swahili language, Unlocked Literal Bible version.

Copyright © 2019 Door43 World Missions Community
Language: Kiswahili (Swahili)
Translation by: Door43 World Missions Community

Contributors: Alfred Danjuma, Bariki Malisa, Christina Abraham Kileo, Cloud Roman, Daniel Marura Chacha, Dina Mast, Dina Roman, Donald Shadarck Dutuyi, Emmanuel Masanja Mbaaga, Emmanuel Nyamalya, Erasmus Peter Malelo, Ev. Lazaro Chalomhola, Ezekiel Manala, Fred, Gabriel Gidale Merus, Gabriel Lwitakubi Mazige, James Makula, James Semnkai, Jeremiah Masasi, Jesse Katabi Masolwa, John Ojasi, Joyce Gilbert Masasi, Karen Riecks, Kazwanomo, Kennedy, Ker, Lameck Yakobo Tobotobo, Laurent Petro Malelo, Lazarus David Chalomhola, Makene Mafwele, Marco Luma Mahushi, Mathew Nkusa, Mathias William, Mr. James Semnkai .It., Musa Isaya Majama, Musa Luzali, Pastor John Kerim, Pastor Jordan, Philipo Mussa Kanwelle, Raphael Musa, Rev. Charles Mabisa, Rev. Yohana Batano, Robert Ndalahwa, Sadiki Kulwa, Samson Nungwana, Thobias Kazwanomo, Yohana Dutuyi, Yohana Magera, Zelote Loilang'akaki Lukumay, Rev. Erasmus Peter Malelo, Ev. Mathew Kazimoto, Rev. Dr. David Magoke, Rev. Elias Ndema, Rev. Alex Nyuri, Rev. Gungutu Elias, Rev. Lameck Tobotobo, Rev. Catherin D. Matia, Rev. Yohana S Dutuyi, Rev. Donald Dutuyi, GS. Andrew Gewe, Ev. Ezekiel Daudi, Rev. John Ndaluka, Ev. Moses Malugu, Rev. Moses Eliakim Ndege, Past. Isack A. Gomugo, Past. Mathias William, Rev. Yekonia M. Koko, Rev. Elisande Mhanga, Ev. James A. Makula.

This translation is made available to you under the terms of the Creative Commons Attribution Share-Alike license 4.0.

You have permission to share and redistribute this Bible translation in any format and to make reasonable revisions and adaptations of this translation, provided that:

  • You include the above copyright and source information.
  • If you make any changes to the text, you must indicate that you did so in a way that makes it clear that the original licensor is not necessarily endorsing your changes.
  • If you redistribute this text, you must distribute your contributions under the same license as the original.

Credits: In addition, we would like to give very special thanks to eBible.org for making Swahili Unlocked Literal Bible available in MySQL format.


Marko 2:1 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Aliporudi Kaperinaumu baada ya siku chache, ilisikika kwamba alikuwa nyumbani.

Marko 2:2 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Watu wengi sana walikuwa wamekusanyika pale na haikuwepo nafasi tena, hata ile ya pale mlangoni, na Yesu alisema neno kwao.

Marko 2:3 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha baadhi ya watu walikuja kwake waliomleta mtu aliyekuwa amepooza; watu wanne walikuwa wamembeba.

Marko 2:4 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakati waliposhindwa kumkaribia kwa sababu ya umati wa watu, waliondoa paa juu ya mahali pale alipokuwa. Na walipokuwa wamekwishatoboa tundu, walishusha kitanda ambacho mtu aliyepooza alikuwa amelala.

Marko 2:5 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Alipoiona imani yao, Yesu alimwambia mtu aliyepooza, “mwanangu, dhambi zako zimesamehewa.”

Marko 2:6 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini baadhi ya waandishi wale waliokuwa wamekaa pale walijihoji mioyoni mwao,

Marko 2:7 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
“Anawezaje mtu huyu kusema hivi? Anakufuru! Nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?”

Marko 2:8 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mara Yesu alijua rohoni mwake walichokuwa wakifikiri miongoni mwao wenyewe. Aliwaambia, “Kwa nini mnafikiri hivi mioyoni mwenu?

Marko 2:9 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lipi ni jepesi zaidi kusema kwa mtu aliyepooza, 'Dhambi zako zimesamehewa' au kusema 'Simama, chukua kitanda chako, na utembee?'

Marko 2:10 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini ili wapate kujua ya kuwa Mwana wa Adamu ana mamlaka ya kusamehe dhambi katika dunia, alimwambia yule aliyepooza,

Marko 2:11 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
“Nakuambia wewe, inuka, chukua mkeka wako, na uende nyumbani kwako.”

Marko 2:12 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Alisimama na mara moja akachukua mkeka wake, na alikwenda nje ya nyumba mbele ya kila mtu, hivyo wote walishangaa na walimpa Mungu utukufu, na wakasema “Kamwe, hatujawahi kuona jambo kama hili.”

Marko 2:13 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Alienda tena kando ya ziwa, na umati wote wa watu walikuja kwake, na akawafundisha.

Marko 2:14 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Alipokuwa akipita alimwona Lawi mwana wa Alfayo ameketi kwenye sehemu ya kukusanyia kodi na akamwambia, “Nifuate.” Alisimama na kumfuata.

Marko 2:15 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Na wakati Yesu alipokuwa akipata chakula katika nyumba ya Lawi, wakusanya kodi wengi na watu wenye dhambi walikuwa wakila na Yesu na wanafunzi wake, kwa kuwa walikuwa wengi nao walimfuata.

Marko 2:16 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakati waandishi, ambao walikuwa Mafarisayo, walipoona kwamba Yesu alikuwa akila na watu wenye dhambi na wakusanya kodi, waliwaambia wanafunzi wake, “Kwa nini anakula na wakusanya kodi na watu wenye dhambi?”

Marko 2:17 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakati Yesu aliposikia hivi aliwaambia, “Watu walio na afya katika mwili hawamhitaji tabibu; ni watu wagonjwa pekee ndio wanamhitaji. Sikuja kuwaita watu wenye haki, lakini watu wenye dhambi.”

Marko 2:18 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wanafunzi wa Yohana na Mafarisayo walikuwa wakifunga. Na baadhi ya watu walikuja kwake na kumwambia, “Kwa nini wanafunzi wa Yohana na mafarisayo hufunga, lakini wanafunzi wako hawafungi?

Marko 2:19 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yesu aliwaambia, “Je waliohudhuria harusini wanaweza kufunga wakati bwana harusi bado akiwa pamoja nao? Kwa vyovyote bwana harusi akiwa bado yuko pamoja nao hawawezi kufunga.”

Marko 2:20 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini siku zitakuja wakati bwana harusi atakapoondolewa kwao, na katika siku hizo wao watafunga.

Marko 2:21 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hakuna mtu ashonaye kipande kipya cha nguo kwenye vazi kuukuu, vinginevyo kiraka kitabanduka kutoka katika hilo, kipya kubanduka kutoka katika kikuukuu, na kutakuwepo mpasuko mbaya.

Marko 2:22 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu, vinginevyo divai itavipasua viriba na vyote viwili divai na viriba vitapotea. Badala yake, weka divai mpya katika viriba vipya.”

Marko 2:23 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Katika siku ya Sabato Yesu alipita kwenye baadhi ya mashamba, na wanafunzi wake walianza kuchukua baadhi ya masuke ya ngano.

Marko 2:24 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Na Mafarisayo walimwambia, “Tazama, kwa nini wanafanya kitu ambacho ni kinyume cha sheria katika siku ya Sabato?”

Marko 2:25 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Aliwaambia, “Hamkusoma kile alichofanya Daudi alipokuwa katika uhitaji na njaa—yeye pamoja na watu waliokuwa pamoja naye?

Marko 2:26 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Jinsi alivyoenda katika nyumba ya Mungu wakati Abiathari alipokuwa kuhani mkuu na akala mkate uliowekwa mbele—ambao ilikuwa kinyume cha sheria kwa mtu yeyote kula isipokuwa makuhani—na aliwapa hata baadhi ya wale waliokuwa pamoja naye?”

Marko 2:27 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yesu alisema, “Sabato ilifanywa kwa ajili ya mwanadamu, siyo mwanadamu kwa ajili ya Sabato.

Marko 2:28 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa hiyo, Mwana wa Adamu ni Bwana, hata kwa Sabato.”
Previous Chapter
« Marko 1 (SWHULB)
Next Chapter
Marko 3 (SWHULB) »

Available Bible Translations

American Standard Version
Mark 2 (ASV) »
King James Version
Mark 2 (KJV) »
GOD’S WORD® (GW)
Mark 2 (GW) »
Berean Bible
Mark 2 (BSB) »
World English Bible
Mark 2 (WEB) »
Louis Segond 1910
Marc 2 (LSG) »
Luther Bibel 1912
Markus 2 (LUTH1912) »
इंडियन रिवाइज्ड वर्जन - हिंदी
मरकुस 2 (HINIRV) »
ਭਾਰਤੀ ਸੋਧਿਆ ਹੋਇਆ ਸੰਸਕਰਣ - ਪੰਜਾਬੀ
ਮਰਕੁਸ 2 (PANIRV) »
ভারতীয় সংশোধিত সংস্করণ - বাংলা
মার্ক 2 (BENIRV) »
இந்தியன் ரீவைஸ்டு வேர்ஷன் - தமிழ்
மாற்கு 2 (TAMIRV) »
इंडियन रिवाइज्ड वर्जन - मराठी
मार्क 2 (MARIRV) »
ఇండియన్ రేవిజ్డ్ వెర్షన్ - తెలుగు
మార్కు 2 (TELIRV) »
ઇન્ડિયન રિવાયઝ્ડ વર્ઝન - ગુજરાતી
માર્ક 2 (GUJIRV) »
ಭಾರತೀಯ ಪರಿಷ್ಕೃತ ಆವೃತ್ತಿ - ಕನ್ನಡ
ಮಾರ್ಕನು 2 (KANIRV) »
الكتاب المقدس باللغة العربية، فان دايك
مَرْقُس 2 (AVD) »
Bíblia Sagrada Português
Marcos 2 (BSL) »
Kinh Thánh: Tiếng Việt
Mác 2 (VIE) »
Reina Valera Antigua
Marcos 2 (RVA) »
La Sacra Bibbia
Marco 2 (RIV) »
圣 经 简体中文和合本
马 可 福 音 2 (CUVS) »
聖 經 繁體中文和合本
馬 可 福 音 2 (CUVT) »
Bibla e Shenjtë
Marku 2 (ALB) »
Svenska Bibeln 1917
Markus 2 (SV1917) »
Библия на русском
Марка 2 (RUSV) »
Українська Біблія
Марка 2 (UKR) »
Szent Biblia - Magyar
Márk 2 (KAR) »
Българска Библия
Марко 2 (BULG) »
Det Norsk Bibel
Markus 2 (NORSK) »
Kitaabka Quduuska Ah
Markos 2 (SOM) »
De Heilige Schrift
Markus 2 (NLD) »
Dansk Bibel 1871
Markus 2 (DA1871) »

Marko (SWHULB) Chapter Selection

1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16

SWHULB Book Selection List