1 Wakorintho 14 SWHULB
1 Wakorintho Chapter 14 SWHULB Bible Verse Images
Copyright © 2019 Door43 World Missions Community
Language: Kiswahili (Swahili)
Translation by: Door43 World Missions Community
Contributors: Alfred Danjuma, Bariki Malisa, Christina Abraham Kileo, Cloud Roman, Daniel Marura Chacha, Dina Mast, Dina Roman, Donald Shadarck Dutuyi, Emmanuel Masanja Mbaaga, Emmanuel Nyamalya, Erasmus Peter Malelo, Ev. Lazaro Chalomhola, Ezekiel Manala, Fred, Gabriel Gidale Merus, Gabriel Lwitakubi Mazige, James Makula, James Semnkai, Jeremiah Masasi, Jesse Katabi Masolwa, John Ojasi, Joyce Gilbert Masasi, Karen Riecks, Kazwanomo, Kennedy, Ker, Lameck Yakobo Tobotobo, Laurent Petro Malelo, Lazarus David Chalomhola, Makene Mafwele, Marco Luma Mahushi, Mathew Nkusa, Mathias William, Mr. James Semnkai .It., Musa Isaya Majama, Musa Luzali, Pastor John Kerim, Pastor Jordan, Philipo Mussa Kanwelle, Raphael Musa, Rev. Charles Mabisa, Rev. Yohana Batano, Robert Ndalahwa, Sadiki Kulwa, Samson Nungwana, Thobias Kazwanomo, Yohana Dutuyi, Yohana Magera, Zelote Loilang'akaki Lukumay, Rev. Erasmus Peter Malelo, Ev. Mathew Kazimoto, Rev. Dr. David Magoke, Rev. Elias Ndema, Rev. Alex Nyuri, Rev. Gungutu Elias, Rev. Lameck Tobotobo, Rev. Catherin D. Matia, Rev. Yohana S Dutuyi, Rev. Donald Dutuyi, GS. Andrew Gewe, Ev. Ezekiel Daudi, Rev. John Ndaluka, Ev. Moses Malugu, Rev. Moses Eliakim Ndege, Past. Isack A. Gomugo, Past. Mathias William, Rev. Yekonia M. Koko, Rev. Elisande Mhanga, Ev. James A. Makula.
This translation is made available to you under the terms of the Creative Commons Attribution Share-Alike license 4.0.
You have permission to share and redistribute this Bible translation in any format and to make reasonable revisions and adaptations of this translation, provided that:
- You include the above copyright and source information.
- If you make any changes to the text, you must indicate that you did so in a way that makes it clear that the original licensor is not necessarily endorsing your changes.
- If you redistribute this text, you must distribute your contributions under the same license as the original.
Credits: In addition, we would like to give very special thanks to eBible.org for making Swahili Unlocked Literal Bible available in MySQL format.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Utafuteni upendo na kutamani sana karama za rohoni, zaidi sana mpate kutoa unabii.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Maana yeye anenaye kwa lugha hasemi na watu bali husema na Mungu. Maana hakuna aelewaye kwa sababu anena mambo yaliyofichika katika Roho.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini yeye atoaye unabii, asema na watu na kuwajenga, kuwatia moyo, na kuwafariji.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yeye anenaye kwa lugha hujijenga mwenyewe, lakini yeye atoaye unabii hulijenga kanisa.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Sasa natamani kwamba ninyi nyote mnene kwa lugha. Lakini zaidi ya hayo, natamani ya kwamba mtoe unabii. Yeye atoaye unabii ni mkuu kuliko yeye anenaye kwa lugha (labda awepo wa kutafasiri), ili kwamba kanisa lipate kujengwa.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini sasa, kaka na dada zangu, nikija kwenu na kunena kwa lugha, nitawafaidia nini ninyi? Siwezi, isipokuwa nasema nanyi kwa njia ya ufunuo, au kwa njia ya maarifa, au unabii, au kwa njia ya fundisho.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ikiwa vitu visivyo na uhai kama filimbi au kinubi visipotoa sauti zilizo na tofauti, itatambulikanaje ni chombo gani kinachezwa?
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa maana ikiwa baragumu itatoa sauti isiyojulikana, ni jinsi gani mtu atatambua ya kuwa ni muda wa kujiandaa kwa vita?
Square Portrait Landscape 4K UHD
Vivyo hivyo na ninyi. Mkitoa kwa ulimi neno lisilo dhahiri, ni jinsi gani mtu ataelewa mnachosema? Mtakuwa mkiongea, na hakuna atakayewaelewa.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hakuna shaka kwamba kuna lugha nyingi mbalimbali duniani, na hakuna hata moja isiyo na maana.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini ikiwa sijui maana ya lugha, nitakuwa mgeni kwake yeye anenaye, naye anenaye atakuwa mgeni kwangu.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Vivyo hivyo na ninyi. Kwa kuwa mnatamani sana kuona uthihirisho wa Roho, takeni kwamba mzidi sana kulijenga kanisa.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hivyo, yeye anenaye kwa lugha na aombe apewe kutafasiri.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa maana nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini akili zangu hazina matunda.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Nifanye nini? Nitaomba kwa roho yangu, lakini pia nitaomba kwa akili zangu. Nitaimba kwa roho yangu, na nitaimba kwa akili zangu pia.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Vinginevyo, ukimsifu Mungu kwa roho, yeye aliye mgeni ataitikaje “Amina” utoapo shukurani, akiwa hayajui usemayo?
Square Portrait Landscape 4K UHD
Maana ni kweli wewe washukuru vema, lakini yule mwingine hajengwi.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Namshukuru Mungu kwa kuwa nanena kwa lugha zaidi ya ninyi nyote.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini katika kanisa ni heri ninene maneno matano kwa ufahamu wangu ili nipate kuwafundisha wengine, zaidi ya kunena maneno kumi elfu kwa lugha.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kaka na dada zangu, msiwe watoto katika kufikiri kwenu. Badala yake, kuhusiana na uovu, iweni kama watoto wachanga. Lakini katika kufikiri kwenu mkawe watu wazima.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Imeandikwa katika sheria, “Kwa watu wa lugha nyingine na kwa midomo ya wageni nitasema na watu hawa. Wala hata hivyo hawatanisikia,” asema Bwana.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hivyo, ndimi ni ishara, sio kwa walioamini, bali kwa wasioamini. Lakini kutoa unabii ni ishara, sio kwa wasioamini, bali kwa ajili yao waaminio.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Haya, ikiwa kanisa lote limekusanyika pamoja na wote wanene kwa lugha, na wageni na wasioamini wameingia, je hawawezi kusema kwamba mna wazimu?
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini ikiwa wote mnatoa unabii na asiyeamini au mgeni akaingia, atashawishiwa na yote asikiayo. Atahukumiwa na yote yasemwayo.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Siri za moyo wake zingefunuliwa. Matokeo yake, angeanguka kifudifudi na kumwabudu Mungu. Angekiri ya kwamba Mungu yu kati yenu.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Nini kifuatacho basi, kaka na dada zangu? Mnapokutana pamoja, kila mmoja ana Zaburi, mafundisho, mafunuo, lugha au tafsiri. Fanyeni kila kitu ili kwamba mlijenge kanisa.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kama yeyote ananena kwa lugha, wawepo wawili au watatu, na kila mmoja katika zamu. Na mtu lazima atafasiri kilichosemwa.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini kama hakuna mtu wa kutafasiri, basi kila mmoja wao akae kimya ndani ya kanisa. Basi kila mmoja aongee peke yake na kwa Mungu.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Na manabii wawili au watatu wanene, na wengine wasikilize kwa kupambanua kilichosemwa.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini aliyeketi akifunuliwa jambo katika huduma, yule ambaye alikuwa ananena na anyamaze.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa kuwa kila mmoja wenu anaweza kutoa unabii mmoja baada ya mwingine ili kwamba kila mmoja aweze kujifunza na wote waweze kutiwa moyo.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa kuwa roho za manabii ziko chini ya uangalizi wa manabii.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa kuwa Mungu si Mungu wa machafuko, bali wa amani. Kama ilivyo katika makanisa yote ya waumini,
Square Portrait Landscape 4K UHD
imewapasa wanawake wakae kimya katika kanisa. Kwa kuwa hawaruhusiwi kuzungumza. Badala yake, wanapaswa kuwa katika unyenyekevu, kama pia sheria inavyosema.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kama kuna chochote wanatamani kujifunza, basi wawaulize waume zao nyumbani. Kwa kuwa ni aibu kwa mwanamke kuongea katika kanisa.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Je neno la Mungu lilitoka kwenu? Je limewafikia ninyi tu?
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kama mtu akijiona kuwa ni nabii au wa rohoni, inampasa ayatambue mambo ninayowaandikia ya kwamba ni maagizo ya Bwana.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini asipotambua haya, mwacheni asitambuliwe.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hivyo basi, kaka na dada zangu, takeni sana kutoa unabii, na msimzuie mtu yeyote kunena kwa lugha.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini mambo yote yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu.
Available Bible Translations
1 Corinthians 14 (ASV) »
1 Corinthians 14 (KJV) »
1 Corinthians 14 (GW) »
1 Corinthians 14 (BSB) »
1 Corinthians 14 (WEB) »
1 Corinthiens 14 (LSG) »
1 Korinther 14 (LUTH1912) »
1 कुरिन्थियों 14 (HINIRV) »
1 ਕੁਰਿੰਥੀਆਂ 14 (PANIRV) »
1 কৰিন্থীয়া 14 (BENIRV) »
1 கொரிந்தியர் 14 (TAMIRV) »
1 करिंथकरांस 14 (MARIRV) »
1 కొరింథీయులకు 14 (TELIRV) »
1 કરિંથીઓને 14 (GUJIRV) »
1 ಕೊರಿಂಥದವರಿಗೆ 14 (KANIRV) »
١ كورنثوس 14 (AVD) »
אגרת שאול הראשונה אל הקורינתים 14 (HEB) »
1 Coríntios 14 (BSL) »
1 Cô-rinh-tô 14 (VIE) »
1 Corintios 14 (RVA) »
1 Corinzi 14 (RIV) »
哥 林 多 前 书 14 (CUVS) »
歌 林 多 前 書 14 (CUVT) »
1 Korintasve 14 (ALB) »
1 Korinthierbrevet 14 (SV1917) »
1 Коринфянам 14 (RUSV) »
1 коринтян 14 (UKR) »
1 Korinthus 14 (KAR) »
1 Коринтяни 14 (BULG) »
コリント人への第一の手紙 14 (JPN) »
1 Korinter 14 (NORSK) »
1 Koryntian 14 (POLUBG) »
1 Korintos 14 (SOM) »
1 Corinthiërs 14 (NLD) »
1 Korintherne 14 (DA1871) »