Yohana 11 SWHULB
Yohana Chapter 11 SWHULB Bible Verse Images
Copyright © 2019 Door43 World Missions Community
Language: Kiswahili (Swahili)
Translation by: Door43 World Missions Community
Contributors: Alfred Danjuma, Bariki Malisa, Christina Abraham Kileo, Cloud Roman, Daniel Marura Chacha, Dina Mast, Dina Roman, Donald Shadarck Dutuyi, Emmanuel Masanja Mbaaga, Emmanuel Nyamalya, Erasmus Peter Malelo, Ev. Lazaro Chalomhola, Ezekiel Manala, Fred, Gabriel Gidale Merus, Gabriel Lwitakubi Mazige, James Makula, James Semnkai, Jeremiah Masasi, Jesse Katabi Masolwa, John Ojasi, Joyce Gilbert Masasi, Karen Riecks, Kazwanomo, Kennedy, Ker, Lameck Yakobo Tobotobo, Laurent Petro Malelo, Lazarus David Chalomhola, Makene Mafwele, Marco Luma Mahushi, Mathew Nkusa, Mathias William, Mr. James Semnkai .It., Musa Isaya Majama, Musa Luzali, Pastor John Kerim, Pastor Jordan, Philipo Mussa Kanwelle, Raphael Musa, Rev. Charles Mabisa, Rev. Yohana Batano, Robert Ndalahwa, Sadiki Kulwa, Samson Nungwana, Thobias Kazwanomo, Yohana Dutuyi, Yohana Magera, Zelote Loilang'akaki Lukumay, Rev. Erasmus Peter Malelo, Ev. Mathew Kazimoto, Rev. Dr. David Magoke, Rev. Elias Ndema, Rev. Alex Nyuri, Rev. Gungutu Elias, Rev. Lameck Tobotobo, Rev. Catherin D. Matia, Rev. Yohana S Dutuyi, Rev. Donald Dutuyi, GS. Andrew Gewe, Ev. Ezekiel Daudi, Rev. John Ndaluka, Ev. Moses Malugu, Rev. Moses Eliakim Ndege, Past. Isack A. Gomugo, Past. Mathias William, Rev. Yekonia M. Koko, Rev. Elisande Mhanga, Ev. James A. Makula.
This translation is made available to you under the terms of the Creative Commons Attribution Share-Alike license 4.0.
You have permission to share and redistribute this Bible translation in any format and to make reasonable revisions and adaptations of this translation, provided that:
- You include the above copyright and source information.
- If you make any changes to the text, you must indicate that you did so in a way that makes it clear that the original licensor is not necessarily endorsing your changes.
- If you redistribute this text, you must distribute your contributions under the same license as the original.
Credits: In addition, we would like to give very special thanks to eBible.org for making Swahili Unlocked Literal Bible available in MySQL format.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Basi mtu mmoja jina lake Lazaro alikuwa mgonjwa. Alitokea Bethania, kijiji cha Mariamu na dada yake Martha.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Alikuwa ni Mariamu yule yule aliyempaka Bwana Marhamu na kumfuta miguu yake kwa nywele zake, ambaye ndugu yake Lazaro alikuwa ni mgonjwa.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo dada hawa walituma ujumbe kwa Yesu na kusema, “Bwana, angalia yule umpendaye anaumwa.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yesu aliposikia alisema, “Ugonjwa huu si wa mauti, lakini, badala yake ni kwa ajili ya utukufu wa Mungu ili kwamba Mwana wa Mungu apate kutukuzwa katika huo Ugonjwa.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Aliposikia kuwa Lazaro ni mgonjwa, Yesu alikaa siku mbili zaidi mahali alipokuwa.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo baada ya hili aliwaambia wanafunzi wake, “Twendeni Uyahudi tena.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wanafunzi wakamwambia, “Rabi, Wayahudi walikuwa wakijaribu kukuponda mawe, na wewe unataka kurudi huko tena?”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yesu akawajibu, “Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu anapotembea mchana hawezi kujikwaa, kwa sababu anaona kwa nuru ya mchana.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hata hivyo, ikiwa atatembea usiku, atajikwaa kwa sababu nuru haiko ndani yake.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yesu akasema mambo haya, na baada ya mambo haya, akawaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini ninakwenda ili kwamba nipate kumuamsha kutoka usingizini.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo wanafunzi wakamwambia, “Bwana, kama amelala, ataamka.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakati huu Yesu alikuwa akizungumza habari za kifo cha Lazaro, lakini wao walidhani anazungumza juu ya kulala usingizi.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo Yesu akazungumza nao wazi wazi, “Lazaro amekufa.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Nina furaha kwa ajili yenu, kwamba sikuwepo kule ili kwamba mpate kuamini. Twendeni kwake.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Basi Tomaso, aliyeitwa Pacha, aliwaambia wanafunzi wenzake, “Nasi twendeni pia tukafe pamoja na Yesu.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakati Yesu alipokuja, alikuta kwamba Lazaro tayari amekwishakuwa kaburini siku nne.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Nayo Bethania ilikuwa karibu na Yerusalemu kama kilomita arobaini na tano hivi.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wengi kati ya Wayahudi wakaja kwa Martha na Mariamu kuwafariji kwa ajili ya ndugu yao.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo Martha aliposikia kuwa Yesu anakuja, alienda kukutana naye, lakini Mariamu aliendelea kukaa nyumbani.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungelikuwa hapa, kaka yangu asingelikufa.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hata sasa, najua ya kuwa lolote utakaloomba kutoka kwa Mungu, atakupatia.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Martha akamwambia, najua kwamba atafufuka katika ufufuo siku ya mwisho.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yesu akamwambia, “Mimi ni ufufuo na uzima; yeye aniaminiye, ingawa atakufa, hata hivyo atakuwa anaishi;
Square Portrait Landscape 4K UHD
na yeye aishiye na kuniamini mimi hatakufa. Unaamini hili?”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akamwambia, “Ndiyo, Bwana naamini kwamba wewe ni Kristo, Mwana wa Mungu, yeye ajaye katika ulimwengu.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Alipokwisha kusema hili, alienda zake na kumwita dada yake Mariamu faraghani. Akasema, “Mwalimu yuko hapa na anakuita.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mariamu aliposikia haya, aliinuka kwa haraka na kwenda kwa Yesu.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Naye Yesu alikuwa hajaja bado ndani ya kijiji, bali alikuwa bado mahali alipokutana na Martha.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo Wayahudi waliokuwa na Mariamu katika nyumba na wale waliokuwa wakimfariji, walipomuona akiinuka haraka na kutoka nje, walimfuata; walidhani kuwa anaenda kaburini ili akalie huko.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo Mariamu, alipofika pale Yesu alipokuwa alimuona na, alianguka chini ya miguu yake na kumwambia, “Bwana, kama ungelikuwa hapa, ndugu yangu asingelikufa.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yesu alipomuona analia, na Wayahudi waliokuja pamoja naye walikuwa wakilia pia, aliomboleza katika roho na kufadhaika;
Square Portrait Landscape 4K UHD
akasema, “Mmemlaza wapi? wakamwambia, Bwana, njoo utazame.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo Wayahudi wakasema, “Angalia alivyompenda Lazaro!”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini wengine kati yao wakasema, “Siyo huyu, mtu aliyeyafumbua macho ya yule aliyekuwa kipofu, hakuweza kumfanya huyu mtu asife?”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo Yesu, hali akiomboleza nafsini mwake tena, alienda kwenye kaburi. Sasa lilikuwa pango, na jiwe limewekwa juu yake.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yesu akasema, “Liondoweni jiwe.” Martha, dada yake na Lazaro, yeye aliyekufa, akamwambia Yesu, “Bwana, kwa muda huu, mwili utakuwa umeoza, kwa sababu amekwishakuwa maiti kwa siku nne.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yesu akamwambia, “Mimi sikukuwaambia ya kwamba, kama ukiamini, utauona utukufu wa Mungu?”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa hiyo wakaliondoa jiwe. Yesu akainua macho yake juu na kusema, “Baba, nakushukuru kwa kuwa unanisikiliza.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Nilijua kwamba unanisikia mara zote, lakini ni kwa sababu ya kusanyiko ambalo limesimama kunizunguka kwamba nimesema haya, ili kwamba wapate kuamini kuwa wewe umenituma.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Baada ya kusema haya, alilia kwa sauti kubwa, “Lazaro, toka nje!”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mfu alitoka nje amefungwa mikono na miguu kwa sanda za kuzikia, na uso wake ulifungwa na kitambaa.” Yesu akawaambia, “Mfungueni mkamwache aende.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo Wayahudi wengi waliokuja kwa Mariamu na kuona Yesu alichofanya, walimwamini;
Square Portrait Landscape 4K UHD
lakini baadhi yao walienda kwa Mafarisayo na kuwaambia mambo aliyoyafanya Yesu.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo wakuu wa Makuhani na Mafarisayo wakakusanyika pamoja katika baraza na kusema, “Tutafanya nini? Mtu huyu anafanya ishara nyingi.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ikiwa tutamwacha hivi peke yake, wote watamwamini; Warumi watakuja na kuchukua vyote mahali petu na taifa letu.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hata hivyo, mtu mmoja kati yao, Kayafa, aliyekuwa kuhani Mkuu mwaka huo, akawaambia, “ Hamjui chochote kabisa.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hamfikirii kwamba yafaa kwa ajili yenu kwamba mtu mmoja yapasa kufa kwa ajili ya watu kuliko taifa lote kuangamia.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Haya hakuyasema kwa sababu yake mwenyewe, badala yake, kwa kuwa alikuwa kuhani mkuu mwaka ule, alitabiri kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa;
Square Portrait Landscape 4K UHD
na si kwa taifa peke yake, bali Yesu apate vile vile kuwakusanya watoto wa Mungu ambao wametawanyika sehemu mbali mbali.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa hiyo kuanzia siku hiyo na kuendelea wakapanga namna ya kumwua Yesu.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yesu hakutembea tena wazi wazi kati ya Wayahudi, bali aliondoka hapo na kwenda nchi iliyo karibu na jangwa katika mji uitwao Efraimu. Hapo alikaa na wanafunzi.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Basi Pasaka ya Wayahudi ilikuwa karibu, na wengi wakapanda kwenda Yerusalemu nje ya mji kabla ya Pasaka ili wapate kujitakasa wenyewe.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Walikuwa wakimtafuta Yesu, na kuzungumza kila mmoja walipokuwa wamesimama hekaluni, “Mnafikiri nini? Kwamba hatakuja katika sikukuu?”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakati huu wakuu wa makuhani na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kwamba ikiwa mmoja atajua Yesu alipo, anapaswa kutoa taarifa ili kwamba wapate kumkamata.
Available Bible Translations
John 11 (ASV) »
John 11 (KJV) »
John 11 (GW) »
John 11 (BSB) »
John 11 (WEB) »
Jean 11 (LSG) »
Johannes 11 (LUTH1912) »
यूहन्ना 11 (HINIRV) »
ਯੂਹੰਨਾ 11 (PANIRV) »
যোহন 11 (BENIRV) »
யோவான் 11 (TAMIRV) »
योहान 11 (MARIRV) »
యోహాను 11 (TELIRV) »
યોહાન 11 (GUJIRV) »
ಯೋಹಾನನು 11 (KANIRV) »
يوحنَّا 11 (AVD) »
הבשורה על־פי יוחנן 11 (HEB) »
João 11 (BSL) »
Giăng 11 (VIE) »
Juan 11 (RVA) »
Giovanni 11 (RIV) »
约 翰 福 音 11 (CUVS) »
約 翰 福 音 11 (CUVT) »
Gjoni 11 (ALB) »
Johannes 11 (SV1917) »
Иоанна 11 (RUSV) »
Івана 11 (UKR) »
János 11 (KAR) »
Йоан 11 (BULG) »
ヨハネによる福音書 11 (JPN) »
Johannes 11 (NORSK) »
Jana 11 (POLUBG) »
Yooxanaa 11 (SOM) »
Johannes 11 (NLD) »
Johannes 11 (DA1871) »