Matendo ya Mitume 5 SWHULB
Matendo ya Mitume Chapter 5 SWHULB Bible Verse Images
Copyright © 2019 Door43 World Missions Community
Language: Kiswahili (Swahili)
Translation by: Door43 World Missions Community
Contributors: Alfred Danjuma, Bariki Malisa, Christina Abraham Kileo, Cloud Roman, Daniel Marura Chacha, Dina Mast, Dina Roman, Donald Shadarck Dutuyi, Emmanuel Masanja Mbaaga, Emmanuel Nyamalya, Erasmus Peter Malelo, Ev. Lazaro Chalomhola, Ezekiel Manala, Fred, Gabriel Gidale Merus, Gabriel Lwitakubi Mazige, James Makula, James Semnkai, Jeremiah Masasi, Jesse Katabi Masolwa, John Ojasi, Joyce Gilbert Masasi, Karen Riecks, Kazwanomo, Kennedy, Ker, Lameck Yakobo Tobotobo, Laurent Petro Malelo, Lazarus David Chalomhola, Makene Mafwele, Marco Luma Mahushi, Mathew Nkusa, Mathias William, Mr. James Semnkai .It., Musa Isaya Majama, Musa Luzali, Pastor John Kerim, Pastor Jordan, Philipo Mussa Kanwelle, Raphael Musa, Rev. Charles Mabisa, Rev. Yohana Batano, Robert Ndalahwa, Sadiki Kulwa, Samson Nungwana, Thobias Kazwanomo, Yohana Dutuyi, Yohana Magera, Zelote Loilang'akaki Lukumay, Rev. Erasmus Peter Malelo, Ev. Mathew Kazimoto, Rev. Dr. David Magoke, Rev. Elias Ndema, Rev. Alex Nyuri, Rev. Gungutu Elias, Rev. Lameck Tobotobo, Rev. Catherin D. Matia, Rev. Yohana S Dutuyi, Rev. Donald Dutuyi, GS. Andrew Gewe, Ev. Ezekiel Daudi, Rev. John Ndaluka, Ev. Moses Malugu, Rev. Moses Eliakim Ndege, Past. Isack A. Gomugo, Past. Mathias William, Rev. Yekonia M. Koko, Rev. Elisande Mhanga, Ev. James A. Makula.
This translation is made available to you under the terms of the Creative Commons Attribution Share-Alike license 4.0.
You have permission to share and redistribute this Bible translation in any format and to make reasonable revisions and adaptations of this translation, provided that:
- You include the above copyright and source information.
- If you make any changes to the text, you must indicate that you did so in a way that makes it clear that the original licensor is not necessarily endorsing your changes.
- If you redistribute this text, you must distribute your contributions under the same license as the original.
Credits: In addition, we would like to give very special thanks to eBible.org for making Swahili Unlocked Literal Bible available in MySQL format.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hivyo, mtu mmoja aliyeitwa Anania, na Safira mkewe, waliuza sehemu ya mali,
Square Portrait Landscape 4K UHD
na akaficha sehemu ya fedha waliyouza (mke wake pia alilijua hili), na akaleta sehemu iliyobakia na kuiweka kwenye miguu ya mitume.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini Petro akasema, “Anania, kwa nini shetani ameujaza moyo wako kusema uongo kwa Roho Mtakatifu na kuficha sehemu ya mali ya shamba?
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakati lilipokuwa halijauzwa, halikuwa ni mali yako? Na baada ya kuuzwa, halikuwa chini ya uamuzi wako? Ilikuwaje uwaze jambo hili moyoni mwako? Hujawadanganya wanadamu, bali umemdanganya Mungu.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Katika kusikia maneno haya, Anania alidondoka chini na akakata roho. Na hofu kubwa iliwajia wote waliolisikia hili.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Vijana wakaja mbele na kumtia katika sanda, na kumpeleka nje na kumzika.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Baada ya masaa matatu hivi, mke wake aliingia ndani, asijue ni nini kilichokuwa kimetokea.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Petro akamwambia, “Niambie, kama mliuza shamba kwa thamani hiyo.” Akasema, “Ndiyo, kwa thamani hiyo.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha Petro akamwambia, “Inakuwaje kwamba mmepatana kwa pamoja kumjaribu Roho wa Bwana? Angalia, miguu ya wale waliomzika mme wako iko mlangoni, na watakubeba na kukupeleka nje.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ghafla akadondoka miguuni pa Petro, akakata roho, na wale vijana wakaja ndani wakamkuta ameshakufa. Wakambeba kumpeleka nje, na kumzika karibu na mmewe.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hofu kubwa ikaja juu ya kanisa zima, na juu ya wote walioyasikia mambo haya.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ishara nyingi na maajabu vilikuwa vinatokea miongoni mwa watu kupitia mikono ya mitume. Walikuwa pamoja katika ukumbi wa Sulemani.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini, hakuna mtu mwingine tofauti aliyekuwa na ujasiri wa kuambatana nao; hata hivyo, walipewa heshima ya juu na watu.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Na pia, waamini wengi walikuwa wakiongezeka kwa Bwana, idadi kubwa ya wanaume na wanawake,
Square Portrait Landscape 4K UHD
kiasi kwamba hata waliwabeba wagonjwa mitaani, na kuwalaza vitandani na kwenye makochi, ili kwamba Petro akiwa anapita, kivuli chake kiweze kushuka juu yao.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hapo pia, idadi kubwa ya watu walikuja kutoka miji iliyozunguka Yerusalem, wakiwaleta wagonjwa na wote waliopagawa na roho wachafu, na wote waliponywa.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini kuhani mkuu aliinuka, na wote waliokuwa pamoja naye (ambao ni wa dhehebu la masadukayo); na walijawa na wivu
Square Portrait Landscape 4K UHD
wakanyosha mikono yao kuwakamata mitume na kuwaweka ndani ya gereza la jumla.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Na wakati wa usiku malaika wa Bwana akaifungua milango ya gereza na kuwaongoza nje na kusema,
Square Portrait Landscape 4K UHD
“Nendeni, mkasimame hekaluni na kuwaambia watu maneno yote ya Uzima huu.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Waliposikia hili, waliingia hekaluni wakati wa kupambazuka na kufundisha. Lakini, kuhani mkuu alikuja na wote waliokuwa naye, na kuitisha baraza lote kwa pamoja, na wazee wote wa watu wa Israeli, na kuwatuma gerezani ili kuwaleta mitume.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini watumishi waliokwenda, hawakuwakuta gerezani, walirudi na kutoa taarifa,
Square Portrait Landscape 4K UHD
“Tumekuta gereza limefungwa vizuri salama, na walinzi wamesimama langoni, lakini tulipokuwa tukifungua, hatukuona mtu ndani.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Sasa wakati jemedari wa hekalu na makuhani wakuu waliposikia maneno haya, waliingiwa na shaka kubwa kwa ajili yao wakiwaza litakuwaje jambo hili.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha mmoja akaja na kuwaambia, “Watu mliowaweka gerezani wamesimama hekaluni na wanafundisha watu.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hivyo jemedari alienda pamoja na watumishi, na wakawaleta, lakini bila ya kufanya vurugu, kwa sababu waliwaogopa watu wangeweza kuwapiga kwa mawe.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Walipokwisha kuwaleta, waliwaweka mbele ya baraza. Kuhani mkuu aliwahoji
Square Portrait Landscape 4K UHD
akisema, “Tuliwaamuru msifundishe kwa jina hili, na bado mmeijaza Yerusalemu kwa fundisho lenu, na kutamani kuleta damu ya mtu huyu juu yetu.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini Petro na mitume wakajibu, “Lazima tumtii Mungu kuliko watu.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mungu wa baba zetu alimfufua Yesu, mliyemuua, kwa kumtundika juu ya mti.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mungu alimtukuza katika mkono wake wa kuume, na kumfanya kuwa Mkuu na mwokozi, kutoa toba kwa Israeli, na msamaha wa dhambi.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Sisi ni mashahidi wa mambo haya, na Roho Mtakatifu, ambaye Mungu amemtoa kwa wale wanaomtii.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wajumbe wa baraza waliposikia hivi, walishikwa na hasira wakataka kuwaua mitume.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini pharisayo aliyeitwa Gamalieli, mwalimu wa sheria, aliyeheshimiwa na watu wote, alisimama na kuwaamuru mitume wachukuliwe nje kwa muda mfupi.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha akawaambia, “Wanaume wa Israeli, iweni makini sana na kile mnachopendekeza kuwafanyia watu hawa.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa sababu, zamani zilizopita, Theuda aliinuka na kujidai kuwa mtu mkuu, na idadi ya watu, wapata mia nne walimfuata. Aliuawa, na wote waliokuwa wanamtii walitawanyika na kupotea.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Baada ya mtu huyu, Yuda mgalilaya, aliinuka siku zile za kuandikwa sensa, akavuta watu wengi nyuma yake. Naye pia alipotea na wote waliokuwa wakimtii walitawanyika.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Sasa nawaambia, jiepusheni na watu hawa na muwaache wenyewe, kwa sababu, kama mpango huu au kazi hii ni ya watu itatupwa.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini kama ni ya Mungu, hamtaweza kuwazuia; mnaweza mkajikuta hata mnashindana na Mungu.” Hivyo, walishawishika na maneno yake.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha, waliwaita mitume ndani na kuwachapa na kuwaamuru wasinene kwa jina la Yesu, na wakawaacha waende zao.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Waliondoka mbele ya baraza wakifurahi kwa sababu wamehesabiwa kuwa wamestahili kuteseka na kutoheshimiwa kwa ajili ya Jina hilo.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa hiyo, kila siku, ndani ya hekalu na kutoka nyumba hadi nyumba waliendelea kufundisha na kuhubiri Yesu kuwa ni Masihi.
Available Bible Translations
Acts 5 (ASV) »
Acts 5 (KJV) »
Acts 5 (GW) »
Acts 5 (BSB) »
Acts 5 (WEB) »
Actes 5 (LSG) »
Apostelgeschichte 5 (LUTH1912) »
प्रेरितों के काम 5 (HINIRV) »
ਰਸੂਲਾਂ ਦੇ ਕਰਤੱਬ 5 (PANIRV) »
पশিষ্যচরিত 5 (BENIRV) »
அப்போஸ்தலருடைய நடபடிகள் 5 (TAMIRV) »
प्रेषितांचीं कृत्यें 5 (MARIRV) »
అపొస్తలుల కార్యములు 5 (TELIRV) »
પ્રેરિતોનાં ક્રત્યો 5 (GUJIRV) »
ಅಪೊಸ್ತಲರ ಕೃತ್ಯಗಳು 5 (KANIRV) »
أَعْمَالُ ٱلرُّسُلِ 5 (AVD) »
מעשי השליחים 5 (HEB) »
Atos 5 (BSL) »
Công Vụ Các Sứ đồ 5 (VIE) »
Hechos 5 (RVA) »
Atti 5 (RIV) »
使 徒 行 传 5 (CUVS) »
使 徒 行 傳 5 (CUVT) »
Veprat e Apostujve 5 (ALB) »
Apostlagärningarna 5 (SV1917) »
Деяния 5 (RUSV) »
Дії 5 (UKR) »
Apostolok 5 (KAR) »
Деяния 5 (BULG) »
使徒行伝 5 (JPN) »
Apostlenes gjerninger 5 (NORSK) »
Dzieje 5 (POLUBG) »
Falimaha Rasuullada 5 (SOM) »
Handelingen 5 (NLD) »
Apostlenes Gerninger 5 (DA1871) »