Mwanzo 30 SWHULB
Mwanzo Chapter 30 SWHULB Bible Verse Images
Copyright © 2019 Door43 World Missions Community
Language: Kiswahili (Swahili)
Translation by: Door43 World Missions Community
Contributors: Alfred Danjuma, Bariki Malisa, Christina Abraham Kileo, Cloud Roman, Daniel Marura Chacha, Dina Mast, Dina Roman, Donald Shadarck Dutuyi, Emmanuel Masanja Mbaaga, Emmanuel Nyamalya, Erasmus Peter Malelo, Ev. Lazaro Chalomhola, Ezekiel Manala, Fred, Gabriel Gidale Merus, Gabriel Lwitakubi Mazige, James Makula, James Semnkai, Jeremiah Masasi, Jesse Katabi Masolwa, John Ojasi, Joyce Gilbert Masasi, Karen Riecks, Kazwanomo, Kennedy, Ker, Lameck Yakobo Tobotobo, Laurent Petro Malelo, Lazarus David Chalomhola, Makene Mafwele, Marco Luma Mahushi, Mathew Nkusa, Mathias William, Mr. James Semnkai .It., Musa Isaya Majama, Musa Luzali, Pastor John Kerim, Pastor Jordan, Philipo Mussa Kanwelle, Raphael Musa, Rev. Charles Mabisa, Rev. Yohana Batano, Robert Ndalahwa, Sadiki Kulwa, Samson Nungwana, Thobias Kazwanomo, Yohana Dutuyi, Yohana Magera, Zelote Loilang'akaki Lukumay, Rev. Erasmus Peter Malelo, Ev. Mathew Kazimoto, Rev. Dr. David Magoke, Rev. Elias Ndema, Rev. Alex Nyuri, Rev. Gungutu Elias, Rev. Lameck Tobotobo, Rev. Catherin D. Matia, Rev. Yohana S Dutuyi, Rev. Donald Dutuyi, GS. Andrew Gewe, Ev. Ezekiel Daudi, Rev. John Ndaluka, Ev. Moses Malugu, Rev. Moses Eliakim Ndege, Past. Isack A. Gomugo, Past. Mathias William, Rev. Yekonia M. Koko, Rev. Elisande Mhanga, Ev. James A. Makula.
This translation is made available to you under the terms of the Creative Commons Attribution Share-Alike license 4.0.
You have permission to share and redistribute this Bible translation in any format and to make reasonable revisions and adaptations of this translation, provided that:
- You include the above copyright and source information.
- If you make any changes to the text, you must indicate that you did so in a way that makes it clear that the original licensor is not necessarily endorsing your changes.
- If you redistribute this text, you must distribute your contributions under the same license as the original.
Credits: In addition, we would like to give very special thanks to eBible.org for making Swahili Unlocked Literal Bible available in MySQL format.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Raheli alipoona kwamba hamzalii Yakobo watoto, Raheli akamwonea wivu dada yake. Akamwambia Yakobo, “Nipe watoto, sivyo nitakufa.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hasira ya Yakobo ikawaka juu ya Raheli. Akasema, “Mimi ni badala ya Mungu, aliyekuzuilia usipate watoto?
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akasema, “Tazama, kuna mjakazi wangu Bilha. Lala naye, hivyo aweze kuzaa watoto magotini pangu, nami nitapata watoto kwake.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hivyo akampa Bilha mjakazi kama mke wake, na Yakobo akalala naye.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Bilha akashika mimba na kumzalia Yakobo mwana.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha Raheli akasema, “Mungu ameamua kwa faida yangu. Ameyasikiliza maombi yangu na kunipa mwana.” Kwa sababu hiyo akamwita jina lake Dani
Square Portrait Landscape 4K UHD
Bilha, mjakazi wa Raheli, akashika mimba tena na kumzalia Yakobo mwana wa pili.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Raheli akasema, “Kwa mashindano yenye nguvu nimeshindana na dada yangu na kushinda.” Akamwita jina lake Naftali.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lea alipoona kwamba ameacha kuzaa, akamchukua Zilpa, mjakazi wake, na kumpa Yakobo kama mke wake.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Zilpa, mjakazi wa Lea, akamzalia Yakobo mwana.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lea akasema, “Hii ni bahati njema!” Hivyo akamwita jina lake Gadi.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha Zilpa, mjakazi wa Lea, akamzalia Yakobo mwana wa pili.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lea akasema, “Nina furaha! Kwa maana mabinti wataniita furaha.” Hivyo akamwita jina lake Asheri.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Siku za mavuno ya ngano Rubeni akaenda shambani na kuona tunguja. Akazileta kwa mama yake. Kisha Raheli akamwambia Lea, “Nipe baadhi ya tunguja za mwanao.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lea akamwambia, “Je ni jambo dogo kwako, kumchukua mme wangu? Je na sasa unataka kuchukua tunguja za mwanangu pia? Raheli akasema, “Kisha atalala nawe leo usiku, kwa kubadilishana na tunguja za mwanao.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Jioni Yakobo akaja kutoka uwandani. Lea akaenda kumlaki na kusema, “Leo usiku utalala nami, kwani nimekuajiri kwa tunguja za mwanangu.” Hivyo Yakobo akalala na Lea usiku huo.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mungu akamsikia Lea, na akashika mimba na kumzalia Yakobo mwana wa tano.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lea akasema, “Mungu amenipa ujira wangu, kwa sababu nilimpa mme wangu mjakazi wangu.” Akamwita jina lake Isakari.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lea akashika mimba tena na kuzaa mwana wa tano kwa Yakobo.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lea akasema, “Mungu amenipa zawadi njema. Sasa mme wangu ataniheshimu, kwa sababu nimemzalia wana sita.” Akamwita jina lake Zabuloni.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Baadaye akazaa binti na kumwita jina lake Dina.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mungu akamkumbuka Raheli na kumsikiliza. Akampa kushika mimba.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akashika mimba na kuzaa mwana. Akasema, “Mungu ameiondoa aibu yangu.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akamwita jina lake Yusufu, akisema, Yahwe ameniongeza mwana mwingine.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Baada ya Raheli kumzaa Yusufu, Yakobo akamwambia Labani, “Niache niande, ili kwamba niende nyumbani kwetu na katika nchi yangu.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Nipe wake zangu na watoto wangu niliokutumikia kwa ajili yao, na uniache niondoke, kwani unafahamu nilivyokutumikia.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Labani akamwambia, “Ikiwa nimepata kibali machoni pako, subiri, kwa sababu nimejifunza kwa kutumia uaguzi kwamba Yahwe amenibariki kwa ajili yako.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha akasema, “Taja ujira wako, nami nitalipa.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yakobo akamwambia, “Unajua nilivyokutumikia, na jinsi ambavyo mifugo wako wamekuwa nami.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwani walikuwa wachache kabla sijaja, na wameongezeka kwa wingi. Popote nilipokutumikia Mungu amekubariki. Je ni lini mimi nitaandaa kwa ajili ya nyumba yangu pia?”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hivyo Labani akasema, “Je nikulipe nini? Yakobo akasema, 'Usinipe chochote. Ikiwa utafanya jambo hili kwa ajili yangu, nitawalisha tena kondoo wako na kuwatunza.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Niache nipite kati ya kundi lako lote leo, kwa kuondoa kila kondoo mwenye milia na mabaka, na kila kondoo mweusi kati yao, na kati ya wenye mabaka na milia katika mbuzi. Hawa watakuwa ujira wangu.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Uadilifu wangu utashuhudia kwa ajili yangu hapo baadaye, utakapokuja kuangalia ujira wangu. Kila ambaye hana milia na hana madoa miongoni mwa mbuzi, na mweusi kati ya kondoo, ikiwa wataonekana kwangu, watahesabiwa kuwa wameibwa.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Labani akasema, “Nakubali. Na iwe kama yalivyo maneno yako.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Siku hiyo Labani akaondoa mabeberu yaliyokuwa na milia na madoa, na majike ya mbuzi yaliyokuwa na milia na madoa, kila aliyekuwa mweupe, na weusi wote katika mbuzi, akawakabidhi katika mikono ya wanaye.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Pia Labani akaweka safari ya siku tatu kati yake na Yakobo. Hivyo Yakobo akabaki kuchunga wale kondoo wa Labani waliosalia.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yakobo akachukua matawi mabichi yaliyokatwa ya mipopla, mlozi na mwaramoni mbichi akatoa maganda ili michilizi myeupe ionekane, na akaifanya sehemu nyeupe ya ndani ya mti iliyokuwa ndani ya fito ionekane.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha akaziweka fito alizokuwa amezibambua mbele ya makundi ya kondoo, mbele ya mabirika yakunyweshea walipokuja kunywa maji. Wakashika mimba walipokuja kunywa maji.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wanyama wakapandana mbele ya fito; nao wakazaa watoto wenye milia, mabaka na wenye madoa.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yakobo akawatenga hawa wanakondoo, lakini akawafanya waliosalia kuelekea wanyama wenye milia na kondoo weusi wote katika kundi la Labani. Kisha akayatenga makundi yake mwenyewe pekee na hakuwaweka pamoja na wale wa Labani.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Pindi kondoo wenye nguvu katika kundi walipopandana, Yakobo alilaza fito katika mabirika ya maji mbele ya macho ya kundi, ili kwamba washike mimba kati ya fito.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini wakati waliodhaifu walipokuja, hakuweka fito mbele yao. Hivyo wanyama dhaifu wakawa wa Labani, na wenye nguvu wakawa wa Yakobo.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mtu huyo akastawi sana. Akawa na kundi kubwa la kondoo, wajakazi na wajoli, ngamia na punda.
Available Bible Translations
Genesis 30 (ASV) »
Genesis 30 (KJV) »
Genesis 30 (GW) »
Genesis 30 (BSB) »
Genesis 30 (WEB) »
Genèse 30 (LSG) »
Genesis 30 (LUTH1912) »
उत्पत्ति 30 (HINIRV) »
ਪੈਦਾਇਸ਼ 30 (PANIRV) »
আদি 30 (BENIRV) »
ஆதியாகமம் 30 (TAMIRV) »
उत्पत्ति 30 (MARIRV) »
ఆదికాండం 30 (TELIRV) »
ઉત્પત્તિ 30 (GUJIRV) »
ಆದಿಕಾಂಡ 30 (KANIRV) »
اَلتَّكْوِينُ 30 (AVD) »
בראשית 30 (HEB) »
Gênesis 30 (BSL) »
Sáng Thế 30 (VIE) »
Génesis 30 (RVA) »
Genesi 30 (RIV) »
创 世 纪 30 (CUVS) »
創 世 記 30 (CUVT) »
Zanafilla 30 (ALB) »
1 Mosebok 30 (SV1917) »
Бытие 30 (RUSV) »
Буття 30 (UKR) »
1 Mózes 30 (KAR) »
Битие 30 (BULG) »
創世記 30 (JPN) »
1 Mosebok 30 (NORSK) »
Rodzaju 30 (POLUBG) »
Bilowgii 30 (SOM) »
Genesis 30 (NLD) »
1 Mosebog 30 (DA1871) »