Mwanzo 42 SWHULB
Mwanzo Chapter 42 SWHULB Bible Verse Images
Copyright © 2019 Door43 World Missions Community
Language: Kiswahili (Swahili)
Translation by: Door43 World Missions Community
Contributors: Alfred Danjuma, Bariki Malisa, Christina Abraham Kileo, Cloud Roman, Daniel Marura Chacha, Dina Mast, Dina Roman, Donald Shadarck Dutuyi, Emmanuel Masanja Mbaaga, Emmanuel Nyamalya, Erasmus Peter Malelo, Ev. Lazaro Chalomhola, Ezekiel Manala, Fred, Gabriel Gidale Merus, Gabriel Lwitakubi Mazige, James Makula, James Semnkai, Jeremiah Masasi, Jesse Katabi Masolwa, John Ojasi, Joyce Gilbert Masasi, Karen Riecks, Kazwanomo, Kennedy, Ker, Lameck Yakobo Tobotobo, Laurent Petro Malelo, Lazarus David Chalomhola, Makene Mafwele, Marco Luma Mahushi, Mathew Nkusa, Mathias William, Mr. James Semnkai .It., Musa Isaya Majama, Musa Luzali, Pastor John Kerim, Pastor Jordan, Philipo Mussa Kanwelle, Raphael Musa, Rev. Charles Mabisa, Rev. Yohana Batano, Robert Ndalahwa, Sadiki Kulwa, Samson Nungwana, Thobias Kazwanomo, Yohana Dutuyi, Yohana Magera, Zelote Loilang'akaki Lukumay, Rev. Erasmus Peter Malelo, Ev. Mathew Kazimoto, Rev. Dr. David Magoke, Rev. Elias Ndema, Rev. Alex Nyuri, Rev. Gungutu Elias, Rev. Lameck Tobotobo, Rev. Catherin D. Matia, Rev. Yohana S Dutuyi, Rev. Donald Dutuyi, GS. Andrew Gewe, Ev. Ezekiel Daudi, Rev. John Ndaluka, Ev. Moses Malugu, Rev. Moses Eliakim Ndege, Past. Isack A. Gomugo, Past. Mathias William, Rev. Yekonia M. Koko, Rev. Elisande Mhanga, Ev. James A. Makula.
This translation is made available to you under the terms of the Creative Commons Attribution Share-Alike license 4.0.
You have permission to share and redistribute this Bible translation in any format and to make reasonable revisions and adaptations of this translation, provided that:
- You include the above copyright and source information.
- If you make any changes to the text, you must indicate that you did so in a way that makes it clear that the original licensor is not necessarily endorsing your changes.
- If you redistribute this text, you must distribute your contributions under the same license as the original.
Credits: In addition, we would like to give very special thanks to eBible.org for making Swahili Unlocked Literal Bible available in MySQL format.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Basi Yakobo akafahamu kwamba kuna nafaka huko Misri. Akawambia wanawe, “Kwa nini mnatazamana?
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akasema, “Tazama, nimesikia kwamba kuna nafaka huko Misri. Shukeni huko mkatununulie chakula ili tuishi wala tusife.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndugu kumi wa Yusufu wakashuka Misri kununua chakula.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini Benjamini, ndugu wa Yusufu, Yakobo hakumtuma na ndugu zake, kwani alihofu kwamba madhara yaweza kumpata.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wana wa Israeli wakaja kununua miongoni mwao waliokuja, kwani njaa ilikuwapo katika nchi ya Kanaani.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Basi Yusufu alikuwa mtawala juu ya nchi. Ndiye aliyekuwa akiwauzia watu wote wa nchi. Ndugu zake Yusufu wakaja na kumwinamia na nyuso zao hata chini.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yusufu akawaona ndugu zake na kuwatambua, lakini alijibadili kwao na kuongea nao kwa ukali. Akawambia, “Mmetoka wapi?” Wakasema, “Kutoka nchi ya Kanaani ili kununua chakula.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yusufu akawatambua ndugu zake, lakini wao hawakumtambua.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yusufu akazikumbuka ndoto aliyoziota kuhusu wao. Akawambia, “Ninyi ni wapelelezi. Mmekuja kuona sehemu za nchi zisizolindwa.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakamwambia, “Hapana, bwana wangu. Watumishi wako wamekuja kununua chakula.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Sisi sote ni wana wa baba mmoja. Ni watu wa kweli. Watumishi wako siyo wapelelezi.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akawambia, “Hapana, mmekuja kuangalia sehemu za nchi zisizolindwa.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakasema, “Sisi watumishi wako tupo ndugu kumi na wawili, wana wa baba mmoja katika nchi ya Kanaani. Tazama, mdogo yupo na baba yetu, na mwingine hayupo hai tena.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yusufu akawambia, “Ndivyo nilivyowambia; ninyi ni wapelelezi.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mtajaribiwa kwa njia hii. Kama aishivyo Farao, hamtaondoka hapa, mdogo wenu asipokuja hapa.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mtumeni mmoja wenu amlete mdogo wenu. Mtabaki gerezani, hata maneno yenu yatakapothibitishwa, kwamba kuna ukweli ndani yenu.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Katika siku ya tatu Yusufu akaongea nao, “Fanyeni hivi nanyi mtaishi, kwani ninamcha Mungu.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kama ninyi ni watu wa kweli, mmoja wenu atazuiliwa hapa gerezani, lakini ninyi nendeni, chukueni nafaka kwa ajili ya nyumba zenu.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mleteni mdogo wenu kwangu ili kwamba maneno yenu yathibitishwe nanyi hamtakufa.” Wakafanya hivyo.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakasemezana wao kwa wao, “Kwa kweli tuna hatia juu ya ndugu yetu kwani tuliona tabu ya nafsi yake alipotusihi nasi hatukusikia. Kwa hiyo taabu hii imeturudia.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Rubeni akawajibu, “Je sikuwambia, 'Msitende dhambi juu ya kijana,' lakini hamkusikia? Basi, tazama, damu yake inatakiwa juu yetu.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini hawakuja kwamba Yusufu anawaelewa, kwani kulikuwa na mkalimani kati yao.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akatoka kwao na kulia. Akarudi kwao na kuongea nao. Akamchukua Simoni miongoni mwao na kumfunga mbele ya macho yao.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha Yusufu akaagiza watumishi kujaza mifuko yao kwa nafaka, na kurudisha pesa ya kila mmoja katika gunia lake, nakuwapa mahitaji kwa safari. Wakatendewa hivyo.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hawa ndugu wakapandisha chakula chao juu ya punda zao na kuondoka pale.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mmoja wao alipofungua gunia lake ili kumlisha punda wao katika sehemu waliyokuwa, akaona pesa yake. Tazama, ilikuwa mdomoni mwa gunia lake.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akawambia ndugu zake, “Pesa yangu imerudishwa. Tazama, imo katika gunia langu.”Mioyo yao ikazimia na wakageukiana kila mmoja huku wakitetemeka. Wakasema, “Ni nini hiki alichotutendea Mungu?”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakaenda kwa Yakobo, baba yao katika nchi ya Kanaani na kumwambia yote yaliyowapata.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakasema, “Yule mtu, bwana wa nchi, aliongea nasi kwa ukali na kutudhania kuwa wapelelezi katika nchi.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Tukamwambia, 'Tu watu wa kweli sisi. Sisi siyo wapelelezi.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Tupo ndugu kumi na wawili, wana wa baba yetu. Mmoja hayupo hai tena, na mdogo yupo na baba yetu katika nchi ya Kanaani.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yule mtu, bwana wa nchi, akatwambia, 'Kwa hili nitajua kwamba ni watu wa kweli ninyi. Mwacheni mmojawapo wa ndugu zenu, chukueni chakula kwa ajili ya njaa katika nyumba zenu, na mwondoke.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mleteni mdogo wenu kwangu. Ndipo nitakapojua kwamba ninyi si wapelelezi, lakini ni watu wa kweli. Kisha nitamwachilia ndugu yenu, na mtafanya biashara katika nchi.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ikawa walipoyafungua magunia yao, na tazama, kila mfuko wa fedha wa mmojawao ulikuwa katika gunia lake. Wakati wao na baba yao walipoona mifuko yao ya fedha, wakaogopa.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yakobo baba yao akawambia, “Mmeniharibia watoto wao. Yusufu hayupo hai tena, Simoni ameondoka, nanyi mmpeleke Benjamini naye. Mambo haya yote ni kunyume changu.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Rubeni akamwambia baba yake, kusema, “Unaweza kuwaua wanangu wawili nisipomrudisha Benjamini kwako. Mweke mikononi mwangu, nami nitamrudisha tena kwako.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yakobo akasema, “Mwanangu atashuka pamoja nanyi. Kwani ndugu yake amekufa na yeye peke yake amebaki. Ikiwa madhara yatampata katika njia mnayoiendea, ndipo mtakapozishusha mvi zangu kaburini kwa huzuni.”
Available Bible Translations
Genesis 42 (ASV) »
Genesis 42 (KJV) »
Genesis 42 (GW) »
Genesis 42 (BSB) »
Genesis 42 (WEB) »
Genèse 42 (LSG) »
Genesis 42 (LUTH1912) »
उत्पत्ति 42 (HINIRV) »
ਪੈਦਾਇਸ਼ 42 (PANIRV) »
আদি 42 (BENIRV) »
ஆதியாகமம் 42 (TAMIRV) »
उत्पत्ति 42 (MARIRV) »
ఆదికాండం 42 (TELIRV) »
ઉત્પત્તિ 42 (GUJIRV) »
ಆದಿಕಾಂಡ 42 (KANIRV) »
اَلتَّكْوِينُ 42 (AVD) »
בראשית 42 (HEB) »
Gênesis 42 (BSL) »
Sáng Thế 42 (VIE) »
Génesis 42 (RVA) »
Genesi 42 (RIV) »
创 世 纪 42 (CUVS) »
創 世 記 42 (CUVT) »
Zanafilla 42 (ALB) »
1 Mosebok 42 (SV1917) »
Бытие 42 (RUSV) »
Буття 42 (UKR) »
1 Mózes 42 (KAR) »
Битие 42 (BULG) »
創世記 42 (JPN) »
1 Mosebok 42 (NORSK) »
Rodzaju 42 (POLUBG) »
Bilowgii 42 (SOM) »
Genesis 42 (NLD) »
1 Mosebog 42 (DA1871) »