Luka Chapter 12 SWHULB Bible Verse Images

Luka 12 Bible Verse Pictures. Choose from a large collection of inspirational, motivational and encouraging Bible verses with pictures of nature. Download and share Luka 12 inspirational Bible verse images. Bible verse pictures were created based on verses from the Swahili Unlocked Literal Bible (SWHULB). The Holy Bible in the Swahili language, Unlocked Literal Bible version.

Copyright © 2019 Door43 World Missions Community
Language: Kiswahili (Swahili)
Translation by: Door43 World Missions Community

Contributors: Alfred Danjuma, Bariki Malisa, Christina Abraham Kileo, Cloud Roman, Daniel Marura Chacha, Dina Mast, Dina Roman, Donald Shadarck Dutuyi, Emmanuel Masanja Mbaaga, Emmanuel Nyamalya, Erasmus Peter Malelo, Ev. Lazaro Chalomhola, Ezekiel Manala, Fred, Gabriel Gidale Merus, Gabriel Lwitakubi Mazige, James Makula, James Semnkai, Jeremiah Masasi, Jesse Katabi Masolwa, John Ojasi, Joyce Gilbert Masasi, Karen Riecks, Kazwanomo, Kennedy, Ker, Lameck Yakobo Tobotobo, Laurent Petro Malelo, Lazarus David Chalomhola, Makene Mafwele, Marco Luma Mahushi, Mathew Nkusa, Mathias William, Mr. James Semnkai .It., Musa Isaya Majama, Musa Luzali, Pastor John Kerim, Pastor Jordan, Philipo Mussa Kanwelle, Raphael Musa, Rev. Charles Mabisa, Rev. Yohana Batano, Robert Ndalahwa, Sadiki Kulwa, Samson Nungwana, Thobias Kazwanomo, Yohana Dutuyi, Yohana Magera, Zelote Loilang'akaki Lukumay, Rev. Erasmus Peter Malelo, Ev. Mathew Kazimoto, Rev. Dr. David Magoke, Rev. Elias Ndema, Rev. Alex Nyuri, Rev. Gungutu Elias, Rev. Lameck Tobotobo, Rev. Catherin D. Matia, Rev. Yohana S Dutuyi, Rev. Donald Dutuyi, GS. Andrew Gewe, Ev. Ezekiel Daudi, Rev. John Ndaluka, Ev. Moses Malugu, Rev. Moses Eliakim Ndege, Past. Isack A. Gomugo, Past. Mathias William, Rev. Yekonia M. Koko, Rev. Elisande Mhanga, Ev. James A. Makula.

This translation is made available to you under the terms of the Creative Commons Attribution Share-Alike license 4.0.

You have permission to share and redistribute this Bible translation in any format and to make reasonable revisions and adaptations of this translation, provided that:

  • You include the above copyright and source information.
  • If you make any changes to the text, you must indicate that you did so in a way that makes it clear that the original licensor is not necessarily endorsing your changes.
  • If you redistribute this text, you must distribute your contributions under the same license as the original.

Credits: In addition, we would like to give very special thanks to eBible.org for making Swahili Unlocked Literal Bible available in MySQL format.


Luka 12:1 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa wakati huo, maelfu mengi ya watu walikusanyika pamoja, kiasi cha kuanza kukanyagana, akaanza kusema na wanafunzi wake kwanza, “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo ambayo ni unafiki”

Luka 12:2 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Na hapatakuwepo na siri iliyofichika ambayo haitafunuliwa, wala jambo lililofichwa ambalo halitajulikana.

Luka 12:3 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Na lolote mlilolisema katika giza, litasikiwa katika mwanga. Na yoyote mliyoyasema kwenye sikio ndani ya vyumba vyenu vya ndani vilivyofungwa yatatangazwa juu ya paa la nyumba.

Luka 12:4 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Nawaambieni rafiki zangu, msiwaogope wale wauao mwili na kisha hawana kitu kingine cha kufanya,

Luka 12:5 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini nitawaonya mtakaye mwogopa. Mwogopeni yule ambaye baada ya kuwa ameua, ana mamlaka ya kutupa jehanamu. Ndiyo, nawaambiani ninyi, mwogopeni huyo.

Luka 12:6 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Je shomoro watano hawauzwi kwa sarafu mbili? hata hivyo hakuna hata mmoja wao atakayesahaulika mbele za Mungu.

Luka 12:7 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini mjue kuwa, nywele za vichwa vyenu vimehesabiwa. Msiogope. Ninyi ni wa thamani kubwa kuliko shomoro wengi.

Luka 12:8 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ninawaambia, yeyote atakayenikiri Mimi mbele za watu, Mwana wa Adamu atamkiri mbele za malaika wa Mungu.

Luka 12:9 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini yeyeyote atakayenikana mbele za watu naye atakanwa mbele ya Malaika wa Mungu.

Luka 12:10 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yeyote atakayesema neno baya juu ya Mwana wa Adamu, atasamehewa, lakini yeyote atakayemkufuru Roho Mtakatifu, hatasamehewa.

Luka 12:11 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Watakapowapeleka mbele za wakuu wa masinagogi, watawala, na wanye mamlaka, msiogope juu na namna ya kuongea katika kujitetea au nini mtakachosema,

Luka 12:12 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
kwa kuwa Roho Mtakatifu atawafundisha namna mtakavyosema kwa wakati huo.”

Luka 12:13 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mtu mmoja katika kusanyiko akamwambia, “Mwalimu, mwambie ndugu yangu anigawie sehemu ya uruthi wangu.”

Luka 12:14 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yesu akamjibu, ni nani aliye niweka kuwa mwamuzi na mpatanishi kati yenu.?

Luka 12:15 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo akawaambia, Jihadharini na kila namna ya tamaa, kwa sababu uzima wa mtu hauko katika wingi wa vitu alivyo navyo.”

Luka 12:16 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yesu akawaambia mfano, akisema, Shamba la mtu mmoja tajiri lilizaa sana,

Luka 12:17 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
na akajiuliza ndani yake, akisema, nitafanyaje kwani sina mahali pa kuhifadhi mazao yangu?

Luka 12:18 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akasema, nitafanya hivi. Nitavunja ghala zangu ndogo na kujenga iliyo kubwa, na kuyahifadhi mazao yangu yote na vitu vingine.

Luka 12:19 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Nitaiambia nafsi yangu, “Nafsi, umejiwekea akiba ya vitu vingi kwa miaka mingi. Pumzika, ule, unywe na kustarehe.”

Luka 12:20 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini Mungu akamwambia, ewe mtu mpumbavu, usiku wa leo wanahitaji roho kutoka kwako, na vitu vyote ulivyoviandaa vitakuwa vya nini?

Luka 12:21 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndivyo itakavyokuwa kwa kila mtu anayejiwekea mali na si kujitajirisha kwa ajili ya Bwana.

Luka 12:22 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yesu akawaambia wanafunzi wake, Kwa hiyo nawaambia msihofu juu ya maisha yenu__ya kuwa mtakula nini au juu ya miili yenu __ya kuwa mtavaa nini

Luka 12:23 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa kuwa maisha ni zaidi ya chakula, na mwili ni zaidi ya mavazi.

Luka 12:24 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Angalieni ndege wa angani, hawalimi wala hawavuni. Hawana chumba wala ghala ya kuhifadhia, lakini Baba yenu huwalisha. Ninyi si bora zaidi kuliko ndege!

Luka 12:25 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ni yupi kati yenu ambaye akijisumbua ataweza kuongeza dhiraa moja katika maisha yake?

Luka 12:26 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ikiwa basi hamuwezi kufanya hicho kitu kidogo kilicho rahisi kwa nini basi kusumbukia hayo mengine?.

Luka 12:27 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Angalieni maua -yanavyomea. Hayafanyi kazi wala hayasokoti. Lakini nawaambia, hata Sulemani katika utukufu wake wote hakuvikwa kama mojawapo ya haya,

Luka 12:28 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kama Mungu huyavika vizuri majani ya kondeni, ambayo leo yapo, na kesho hutupwa kwenye moto. Je si zaidi atawavika ninyi? enyi wa imani haba!

Luka 12:29 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Msisumbukie juu ya kuwa mtakula nini au mtakunywa nini, wala msiwe na hofu.

Luka 12:30 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa kuwa Mataifa yote ya dunia husumbukia mambao yao. Na Baba yenu anajua ya kuwa mnahitaji hayo.

Luka 12:31 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini tafuteni ufalme wake kwanza, na hayo mengine mtazidishiwa,

Luka 12:32 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
msiogope, enyi kundi dogo, kwa sababu Baba yenu anafurahia kuwapa ninyi huo ufalme.

Luka 12:33 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Uzeni mali zenu na mkawape maskini, mjifanyie mifuko isiyoishiwa__hazina ya mbinguni isiyokoma, sehemu ambapo wezi hawatakaribia wala nondo haitaweza kuharibu.

Luka 12:34 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa kuwa palipo na hazina yako, ndipo na roho yako itakapokuwepo.

Luka 12:35 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Nguo zenu ndefu ziwe zimefungwa kwa mkanda, na taa zenu zihakikishwe kuwa zinaendelee kuwaka,

Luka 12:36 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
na muwe kama watu wanaomtazamia Bwana wao kutoka kwenye sherehe ya harusi, ili kwamba akija na kupiga hodi, wataweze kumfungulia mlango kwa haraka.

Luka 12:37 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wamebarikiwa wale watumishi, ambao Bwana atawakuta wako macho. Hakika atafunga nguo yake ndefu kwa mkanda, kisha atawaketisha chini kwa chakula, na kisha kuwahudumia.

Luka 12:38 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kama Bwana atakuja kwa zamu ya pili ya ulinzi ya usiku, au hata zamu ya tatu ya ulinzi, na kuwakuta wakiwa tayari, itakuwa ni heri kwa hao watumishi.

Luka 12:39 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Zaidi ya hayo, mjue hili, kama bwana mwenye nyumba angelijua saa ambayo mwivi anakuja, asingeliruhusu nyumba yake ifunjwe.

Luka 12:40 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Iweni tayari pia kwani hamjui ni wakati gani mwana wa Adamu atarudi.

Luka 12:41 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Petro akasema, “Bwana, watuambia sisi wenyewe hii mifano, au unamwambia kila mtu.?

Luka 12:42 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Bwana akawaambia, “Ni nani mtumwa mwaminifu au mwenye hekima ambaye bwana wake atamweka juu ya watumishi wengine, ili awagawie chakula chao kwa wakati mwafaka?

Luka 12:43 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Amebarikiwa mtumishi yule, ambaye bwana wake akija atamkuta akifanya yale aliyoagizwa.

Luka 12:44 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hakika nawaambia ninyi ya kuwa atamweka juu ya mali yake yote.

Luka 12:45 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini Mtumishi yule akisema moyoni mwake, “bwana wangu anachelewa kurudi; hivyo akaanza kuwapiga wale watumishi wa kiume na wa kike, kisha akaanza kula, kunywa na kulewa,

Luka 12:46 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
bwana wake yule mtumwa atakuja katika siku asiyotegemea na saa asiyoijua, naye atamkata vipande vipande na kumuweka katika sehemu pamoja na wasiokuwawaaminifu'

Luka 12:47 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mtumishi, anayejua mapenzi ya bwana wake, naye hakujiandaaa wala hakufanya sawa sawa na mapenzi yake, atapigwa viboko vingi.

Luka 12:48 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini mtumishi asiyejua mapenzi ya bwana wake, lakini akafanya yanayostahili adhabu, atapigwa viboko vichache. Kwa kuwa yeye aliyepewa vingi, vingi hudaiwa kutoka kwake, na yeye aliyeaminiwa kwa vingi, kwake vitadaiwa vingi zaidi.

Luka 12:49 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Nimekuja kuwasha moto duniani, na natamani iwe umekwishawaka,

Luka 12:50 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini nina ubatizo ambao nitabatizwa, na nina huzuni mpaka utkapokamilika!

Luka 12:51 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Je mnafikiri kuwa nimekuja kuleta amani duniani? Hapana, Nawaambieni, badala yake nimeleta mgawanyiko.

Luka 12:52 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Tangu sasa na kuendelea kutakuwa na watu watano katika nyumba moja wamegawanyika, na watatu watakuwa kinyume na wawili, na wawili watakuwa kinyume na watatu.

Luka 12:53 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Watagawanyika, baba atakuwa kinyume na mwanae, na mwanae atakuwa kinyume na babaye, mama atakuwa kinyume na binti yake, na binti atakuwa kinyume na mama yake, Mama mkwe atakuwa kinyume na mkwe wake naye mkwe atakuwa kinyume na mama mkwe wake.

Luka 12:54 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yesu akawa anawaambia makutano pia, “Mara muonapo mawingu yakitokea magharibi, mnasema nyakati za mvua zimewadia; na ndivyo inavyo kuwa,

Luka 12:55 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Na upepo wa kusini ukivuma, mnasema, Patakuwepo na joto kali, na ndivyo inavyokuwa.

Luka 12:56 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Enyi wanafiki, mnaweza kutafsiri mwonekano wa nchi na anga, lakini inakuwaje hamuwezi kuutafsiri wakati uliopo?

Luka 12:57 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ni kwa nini kila mmoja wenu asipambanue lililo sahihi kwake kulifanya wakati ambapo angali na nafasi ya kufanya hivyo?

Luka 12:58 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Maana mkienda na mshitaki wako mbele ya hakimu, jitahidi kupatana na mshitaki wako mungali bado mko njiani asije akakupeleka kwa hakimu, na hakimu akupeleka kwa ofisa, na ofisa akakutupa gerezani.

Luka 12:59 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Nakuambia, hutatoka huko hadi umelipa mpaka senti ya mwisho.
Previous Chapter
« Luka 11 (SWHULB)
Next Chapter
Luka 13 (SWHULB) »

Available Bible Translations

American Standard Version
Luke 12 (ASV) »
King James Version
Luke 12 (KJV) »
GOD’S WORD® (GW)
Luke 12 (GW) »
Berean Bible
Luke 12 (BSB) »
World English Bible
Luke 12 (WEB) »
Louis Segond 1910
Luc 12 (LSG) »
Luther Bibel 1912
Lukas 12 (LUTH1912) »
इंडियन रिवाइज्ड वर्जन - हिंदी
लूका 12 (HINIRV) »
ਭਾਰਤੀ ਸੋਧਿਆ ਹੋਇਆ ਸੰਸਕਰਣ - ਪੰਜਾਬੀ
ਲੂਕਾ 12 (PANIRV) »
ভারতীয় সংশোধিত সংস্করণ - বাংলা
লূক 12 (BENIRV) »
இந்தியன் ரீவைஸ்டு வேர்ஷன் - தமிழ்
லூக்கா 12 (TAMIRV) »
इंडियन रिवाइज्ड वर्जन - मराठी
लूक 12 (MARIRV) »
ఇండియన్ రేవిజ్డ్ వెర్షన్ - తెలుగు
లూకా 12 (TELIRV) »
ઇન્ડિયન રિવાયઝ્ડ વર્ઝન - ગુજરાતી
લૂક 12 (GUJIRV) »
ಭಾರತೀಯ ಪರಿಷ್ಕೃತ ಆವೃತ್ತಿ - ಕನ್ನಡ
ಲೂಕನು 12 (KANIRV) »
الكتاب المقدس باللغة العربية، فان دايك
لُوقا 12 (AVD) »
Bíblia Sagrada Português
Lucas 12 (BSL) »
Kinh Thánh: Tiếng Việt
Lu-ca 12 (VIE) »
Reina Valera Antigua
Lucas 12 (RVA) »
La Sacra Bibbia
Luca 12 (RIV) »
圣 经 简体中文和合本
路 加 福 音 12 (CUVS) »
聖 經 繁體中文和合本
路 加 福 音 12 (CUVT) »
Bibla e Shenjtë
Luka 12 (ALB) »
Svenska Bibeln 1917
Lukas 12 (SV1917) »
Библия на русском
Луки 12 (RUSV) »
Українська Біблія
Луки 12 (UKR) »
Szent Biblia - Magyar
Lukács 12 (KAR) »
Българска Библия
Лука 12 (BULG) »
Det Norsk Bibel
Lukas 12 (NORSK) »
Kitaabka Quduuska Ah
Luukos 12 (SOM) »
De Heilige Schrift
Lukas 12 (NLD) »
Dansk Bibel 1871
Lukas 12 (DA1871) »

Luka (SWHULB) Chapter Selection

SWHULB Book Selection List