Luka 23 SWHULB
Luka Chapter 23 SWHULB Bible Verse Images
Copyright © 2019 Door43 World Missions Community
Language: Kiswahili (Swahili)
Translation by: Door43 World Missions Community
Contributors: Alfred Danjuma, Bariki Malisa, Christina Abraham Kileo, Cloud Roman, Daniel Marura Chacha, Dina Mast, Dina Roman, Donald Shadarck Dutuyi, Emmanuel Masanja Mbaaga, Emmanuel Nyamalya, Erasmus Peter Malelo, Ev. Lazaro Chalomhola, Ezekiel Manala, Fred, Gabriel Gidale Merus, Gabriel Lwitakubi Mazige, James Makula, James Semnkai, Jeremiah Masasi, Jesse Katabi Masolwa, John Ojasi, Joyce Gilbert Masasi, Karen Riecks, Kazwanomo, Kennedy, Ker, Lameck Yakobo Tobotobo, Laurent Petro Malelo, Lazarus David Chalomhola, Makene Mafwele, Marco Luma Mahushi, Mathew Nkusa, Mathias William, Mr. James Semnkai .It., Musa Isaya Majama, Musa Luzali, Pastor John Kerim, Pastor Jordan, Philipo Mussa Kanwelle, Raphael Musa, Rev. Charles Mabisa, Rev. Yohana Batano, Robert Ndalahwa, Sadiki Kulwa, Samson Nungwana, Thobias Kazwanomo, Yohana Dutuyi, Yohana Magera, Zelote Loilang'akaki Lukumay, Rev. Erasmus Peter Malelo, Ev. Mathew Kazimoto, Rev. Dr. David Magoke, Rev. Elias Ndema, Rev. Alex Nyuri, Rev. Gungutu Elias, Rev. Lameck Tobotobo, Rev. Catherin D. Matia, Rev. Yohana S Dutuyi, Rev. Donald Dutuyi, GS. Andrew Gewe, Ev. Ezekiel Daudi, Rev. John Ndaluka, Ev. Moses Malugu, Rev. Moses Eliakim Ndege, Past. Isack A. Gomugo, Past. Mathias William, Rev. Yekonia M. Koko, Rev. Elisande Mhanga, Ev. James A. Makula.
This translation is made available to you under the terms of the Creative Commons Attribution Share-Alike license 4.0.
You have permission to share and redistribute this Bible translation in any format and to make reasonable revisions and adaptations of this translation, provided that:
- You include the above copyright and source information.
- If you make any changes to the text, you must indicate that you did so in a way that makes it clear that the original licensor is not necessarily endorsing your changes.
- If you redistribute this text, you must distribute your contributions under the same license as the original.
Credits: In addition, we would like to give very special thanks to eBible.org for making Swahili Unlocked Literal Bible available in MySQL format.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mkutano wote wakasimama, wakampeleka Yesu mbele ya Pilato.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakaanza kumshutumu, wakisema, “Tumemkuta mtu huyu akipotosha taifa letu, kwa kukataza tusitoe kodi kwa Kaisari, na akisema kwamba yeye mwenyewe ni Kristo, Mfalme.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Pilato akamuuliza, akisema, “Je wewe ni Mfalme wa Wayahudi?” Na Yesu akamjibu akisema, “Wewe wasema hivyo”.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Pilato akamuambia kuhani mkuu na makutano, “Sioni kosa kwa mtu huyu”.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini wao wakasisitiza, wakisema, “ Amekuwa akiwachochea watu, akifundisha katika Uyahudi yote, kuanzia Galilaya na sasa yuko hapa.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Pilato aliposikia haya, akaulizia kama mtu huyo ni wa Galilaya?
Square Portrait Landscape 4K UHD
Alipotambua kuwa alikuwa chini ya utawala wa Herode, akampeleka Yesu kwa Herode, ambaye naye alikuwa Yerusalemu kwa siku hizo.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Herode alipomuona Yesu, alifurahi sana kwasababu alitaka kumuona kwa siku nyingi. Alisikia habari zake na alitamani kuona moja ya miujiza ikifanywa na yeye.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Herode alimhoji Yesu kwa maneno mengi, lakini Yesu hakumjibu chochote.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Makuhani wakuu pamoja na waandishi walisimama kwa ukali wakimshitaki.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Herode pamoja na maaskari wake, walimtukana na kumdhihaki, na kumvika mavazi mazuri, kisha akamrudisha Yesu kwa Pilato.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Herode na Pilato wakawa marafiki kuanzia siku hiyo, (kabla ya hapo walikuwa maadui).
Square Portrait Landscape 4K UHD
Pilato akawaita pomoja makuhani wakuu na watawala na umati wa watu,
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akawaambia, “Mmeniletea mtu huyu kama mtu anaye waongoza watu wafanye mabaya, na tazama, baada ya kuwa nimemhoji mbele yenu, sikuona kosa kwa mtu huyu kuhusu mambo yote ambayo ninyi mnamshitaki yeye.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hapana, wala Herode, kwa maana amemrudisha kwetu, na tazama hakuna chochote alichokifanya kinachostahili adhabu ya kifo.
Square Portrait Landscape 4K UHD
(Sasa, Pilato anawajibika kumuachilia mfungwa mmoja kwa wayahudi wakati wa sikukuu).
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini wote wakapiga kelele pamoja, wakisema, “Mwondoe huyo, na tufungulie Baraba!”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Baraba alikuwa ni mtu ambaye amewekwa gerezani kwa sababu ya uasi fulani katika jiji na kwa kuua.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Pilato akawaambia tena, akitamani kumwachilia Yesu.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini wao wakapiga kelele, wakisema, “Msulibishe, msulibishe.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akawauliza kwa mara ya tatu, “kwa nini, huyu mtu amefanya maovu gani? Sikupata kosa linalostahili adhabu ya kifo kwake. Kwahiyo nitakapo maliza kumuadhibu nitamuachilia.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini wakasisitiza kwa sauti ya juu, wakitaka asulubiwe. Na sauti zao zikamshawishi Pilato.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akamuachilia yule waliyemtaka ambaye alifungwa kwa kusababisha ghasia na kuua. Lakini akamtoa Yesu kwa matakwa yao.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Walipokuwa wakimpeleka, walimkamata mtu mmoja aitwaye Simoni wa Ukirene, akitokea katika nchi, wakamtwika msalaba ili abebe, akimfuata Yesu.
Square Portrait Landscape 4K UHD
umati mkubwa wa watu, na wanawake ambao walihuzunika na kuomboleza kwa ajili yake, walikuwa wakimfuata.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini akawageukia, Yesu akawaambia, 'Mabinti wa Yerusalemu, msinililie mimi, bali jililieni ninyi wenyewe na kwa ya ajili watoto wenu.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Tazama, siku zinakuja ambazo watasema, “Wamebarikiwa walio tasa na matumbo yasiyozaa, na matiti ambayo hayakunyonyesha.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo watakapo anza kuiambia milima, 'Tuangukieni,' na vilima, 'Mtufunike.'
Square Portrait Landscape 4K UHD
Maana kama wakifanya mambo haya ikiwa mti mbichi, itakuwaje ukiwa mkavu?”
Square Portrait Landscape 4K UHD
wanaume wengine, wahalifu wawili, walipelekwa pamoja naye ili wauwawe.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Walipofika mahali paitwapo Fuvu la kichwa, ndipo wakamsulubisha pamoja na wale wahalifu, mmoja upande wa kulia na mwingine upande wa kushoto.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yesu alisema, “Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. “Nao wakapiga kura, kugawa mavazi yake.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Watu walikuwa wamesimama wakiangalia huku watawala wakimdhihaki, wakisema, “Aliwaokoa wengine. Sasa ajiokoe mwenyewe, kama yeye ni Kristo wa Mungu, mteule”.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Askari pia walimdharau, walimkaribia yeye na wakumpa siki,
Square Portrait Landscape 4K UHD
wakisema, “Kama wewe ni Mfalme wa Wayahudi jiokoe mwenyewe”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kulikuwa pia na alama juu yake iliyoandikwa “HUYU NDIYE MFALME WA WAYAHUDI.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mmoja wa wahalifu aliyesulubishwa alimtukana akisema, “Wewe si Kristo? jiokoe mwenyewe na sisi”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini yule mwingine akajibu, akimkemea na akisema, “Je wewe humuogopi Mungu, nawe uko katika hukumu hiyo hiyo?
Square Portrait Landscape 4K UHD
Sisi tupo hapa kwa haki, kwa maana sisi tunapokea kile tunachostahili kwa matendo yetu. Lakini mtu huyu hakufanya chochote kibaya.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Na aliongeza, “Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yesu akamwambia, “Amini nakuambia, leo hii utakuwa pamoja nami Paradiso.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hapo ilikuwa karibu saa ya sita, giza likaja juu ya nchi yote hadi saa ya tisa,
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mwanga wa jua ulizimika. Kisha pazia la hekalu likagawanyika katikati kuanzia juu.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akilia kwa sauti kuu, Yesu alisema, “Baba mikononi mwako naiweka roho yangu,” baada ya kusema haya, akafa.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakati Akida alipoona yaliyotendeka alimtukuza Mungu akisema, “Hakika huyu alikuwa mtu mwenye haki.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakati umati wa watu waliokuja pamoja kushuhudia walipoona mambo yaliyofanyika, walirudi huku wakipiga vifua vyao.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini marafiki zake, na wanawake waliomfuata toka Galilaya, walisimama kwa mbali wakiangalia hayo mambo.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Tazama, palikuwepo na mtu aitwaye Yusufu, ambaye ni mmoja wa baraza, mtu mzuri na mwenye haki,
Square Portrait Landscape 4K UHD
(alikuwa hajakubaliana na maamuzi au matendo yao), kutoka Armathaya, mji wa Kiyahudi, ambao ulikua ukisubiria ufalme wa Mungu.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mtu huyu, alimkaribia Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Alimshusha, na akauzungushia sanda, na akaumweka katika kaburi lililokuwa limechongwa katika jiwe, ambalo hakuna aliyewahi kuzikwa.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ilikuwa ni siku ya maandalizi, na Sabato inakaribia.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wanawake, waliokuja nao kutoka Galilaya, walimfuata, na wakaona kaburi na jinsi mwili wake ulivyolazwa.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Walirudi na kuanza kuandaa manukato na marashi. Kisha siku ya sabato walipumzika kwa mujibu wa sheria.
Available Bible Translations
Luke 23 (ASV) »
Luke 23 (KJV) »
Luke 23 (GW) »
Luke 23 (BSB) »
Luke 23 (WEB) »
Luc 23 (LSG) »
Lukas 23 (LUTH1912) »
लूका 23 (HINIRV) »
ਲੂਕਾ 23 (PANIRV) »
লূক 23 (BENIRV) »
லூக்கா 23 (TAMIRV) »
लूक 23 (MARIRV) »
లూకా 23 (TELIRV) »
લૂક 23 (GUJIRV) »
ಲೂಕನು 23 (KANIRV) »
لُوقا 23 (AVD) »
הבשורה על־פי לוקס 23 (HEB) »
Lucas 23 (BSL) »
Lu-ca 23 (VIE) »
Lucas 23 (RVA) »
Luca 23 (RIV) »
路 加 福 音 23 (CUVS) »
路 加 福 音 23 (CUVT) »
Luka 23 (ALB) »
Lukas 23 (SV1917) »
Луки 23 (RUSV) »
Луки 23 (UKR) »
Lukács 23 (KAR) »
Лука 23 (BULG) »
ルカによる福音書 23 (JPN) »
Lukas 23 (NORSK) »
Łukasza 23 (POLUBG) »
Luukos 23 (SOM) »
Lukas 23 (NLD) »
Lukas 23 (DA1871) »