Luka 22 SWHULB
Luka Chapter 22 SWHULB Bible Verse Images
Copyright © 2019 Door43 World Missions Community
Language: Kiswahili (Swahili)
Translation by: Door43 World Missions Community
Contributors: Alfred Danjuma, Bariki Malisa, Christina Abraham Kileo, Cloud Roman, Daniel Marura Chacha, Dina Mast, Dina Roman, Donald Shadarck Dutuyi, Emmanuel Masanja Mbaaga, Emmanuel Nyamalya, Erasmus Peter Malelo, Ev. Lazaro Chalomhola, Ezekiel Manala, Fred, Gabriel Gidale Merus, Gabriel Lwitakubi Mazige, James Makula, James Semnkai, Jeremiah Masasi, Jesse Katabi Masolwa, John Ojasi, Joyce Gilbert Masasi, Karen Riecks, Kazwanomo, Kennedy, Ker, Lameck Yakobo Tobotobo, Laurent Petro Malelo, Lazarus David Chalomhola, Makene Mafwele, Marco Luma Mahushi, Mathew Nkusa, Mathias William, Mr. James Semnkai .It., Musa Isaya Majama, Musa Luzali, Pastor John Kerim, Pastor Jordan, Philipo Mussa Kanwelle, Raphael Musa, Rev. Charles Mabisa, Rev. Yohana Batano, Robert Ndalahwa, Sadiki Kulwa, Samson Nungwana, Thobias Kazwanomo, Yohana Dutuyi, Yohana Magera, Zelote Loilang'akaki Lukumay, Rev. Erasmus Peter Malelo, Ev. Mathew Kazimoto, Rev. Dr. David Magoke, Rev. Elias Ndema, Rev. Alex Nyuri, Rev. Gungutu Elias, Rev. Lameck Tobotobo, Rev. Catherin D. Matia, Rev. Yohana S Dutuyi, Rev. Donald Dutuyi, GS. Andrew Gewe, Ev. Ezekiel Daudi, Rev. John Ndaluka, Ev. Moses Malugu, Rev. Moses Eliakim Ndege, Past. Isack A. Gomugo, Past. Mathias William, Rev. Yekonia M. Koko, Rev. Elisande Mhanga, Ev. James A. Makula.
This translation is made available to you under the terms of the Creative Commons Attribution Share-Alike license 4.0.
You have permission to share and redistribute this Bible translation in any format and to make reasonable revisions and adaptations of this translation, provided that:
- You include the above copyright and source information.
- If you make any changes to the text, you must indicate that you did so in a way that makes it clear that the original licensor is not necessarily endorsing your changes.
- If you redistribute this text, you must distribute your contributions under the same license as the original.
Credits: In addition, we would like to give very special thanks to eBible.org for making Swahili Unlocked Literal Bible available in MySQL format.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Basi Sikukuu ya Mkate Usiyotiwa Chachu ilikuwa imekaribia, ambayo inaitwa Pasaka.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Makuhani wakuu na waandishi wakajadiliana namna ya kumuua Yesu, kwa sababu waliwaogopa watu.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Shetani akaingia ndani ya Yuda Iskariote, mmoja wa wale wanafunzi Kumi na mbili.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yuda akaenda kujadiliana na wakuu wa makuhani na wakuu namna ambavyo atamkabidhi Yesu kwao.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yeye aliridhia, na alitafuta fursa ya kumkabidhi Yesu kwao mbali na kundi la watu.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Siku ya mikate isiyotiwa chachu ikafika, ambapo kondoo wa Pasaka lazima atolewe.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yesu akawatuma Petro na Yohana, akasema, “Nendeni mkatuandalie chakula cha Pasaka ili tuje tukile.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakamuuliza, “Wapi unataka tuyafanyie hayo maandalizi?”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akawajibu, “Sikilizeni, mtakapokuwa mmeingia mjini, mwanamume ambaye amebeba mtungi wa maji atakutana na ninyi. Mfuateni kwenye nyumba ambayo ataingia.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha mwambieni bwana wa nyumba, “Mwalimu anakwambia, “Kiko wapi chumba cha wageni, mahali ambapo nitakula Pasaka na wanafunzi wangu?”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Atawaonyesha chumba cha ghorofani ambacho kiko tayari. Fanyeni maandalizi humo.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hivyo wakaenda, na wakakuta kila kitu kama alivyowaambia. Kisha wakaandaa chakula cha Pasaka.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha akawaambia, “Nina shauku kubwa ya kula sikukuu hii ya Pasaka na ninyi kabla ya kuteswa kwangu.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa maana nawaambieni, sitakula tena mpaka itakapotimizwa katika ufalme wa Mungu.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha Yesu akachukua kikombe, na alipokwisha kushukuru, akasema, “Chukueni hiki, na mgawane ninyi kwa ninyi.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa maana nawaambia, sitakunywa tena mzao wa mzabibu, mpaka ufalme wa Mungu utakapokuja.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha akachukua mkate, na alipokwisha kushukuru, akaumega, na kuwapa, akisema, “Huu ni mwili wangu ambao umetolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka mimi.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akachukua kikombe vivyo hivyo baada ya chakula cha usiku akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu, ambayo imemwagika kwa ajili yenu.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini angalieni. Yule anisalitie yuko pamoja nami mezani.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa maana Mwana wa Adamu kwa kweli aenda zake kama ilivyokwisha amuliwa. Lakini ole kwa mtu yule ambaye kupitia yeye Mwana wa Adamu asalitiwa!”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakaanza kuulizana wao kwa wao, nani miongoni mwao ambaye angefanya jambo hili.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha yakatokea mabishano katikati yao kwamba ni nani anaye dhaniwa kuwa mkuu kuliko wote.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akawaambia, “Wafalme wa watu wa mataifa wana ubwana juu yao, na wale mwenye mamlaka juu yao wanaitwa waheshimiwa watawala.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini haitakiwi kabisa kuwa hivi kwenu ninyi. Badala yake, acha yule ambaye ni mkubwa kati yenu awe kama mdogo. Na yule ambaye ni wa muhimu sana awe kama atumikaye.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa sababu yupi mkubwa, yule akaaye mezani au yule anayetumika? Je si yule aketie mezani? Na mimi bado ni kati yenu kama atumikaye.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini ninyi ndio ambao mmeendelea kuwa nami katika majaribu yangu.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Nawapa ninyi ufalme, kama vile Baba alivyonipa mimi ufalme,
Square Portrait Landscape 4K UHD
kwamba mpate kula na kunywa mezani kwangu kwenye ufalme wangu. Na mtakaa kwenye viti vya enzi mkizihukumu kabila kumi na mbili za Israel.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Simoni, Simoni, fahamu kwamba, Shetani ameomba awapate ili awapepete kama ngano.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini nimekuombea, kwamba imani yako isishindwe. Baada ya kuwa umerudi tena, waimarishe ndugu zako.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Petro akamwambia, “Bwana, niko tayari kwenda na wewe gerezani na hata katika mauti.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yesu akajibu, “Nakwambia, Petro, Jogoo hatawika leo, kabla hujanikana mara tatu kwamba unanijua.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha Yesu akawaambia, “Nilipowapeleka ninyi bila mfuko, kikapu cha vyakula, ua viatu, je mlipungukiwa na kitu?” Wakajibu “Hakuna.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha akawaambia, “Lakini sasa, kila mwenye mfuko, na auchukue pamoja na kikapu cha vyakula. Yule ambaye hana upanga imempasa auze joho lake anunue mmoja.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa sababu nawaambia, yote ambayo yameandikwa kwa ajili yangu lazima yatimilike, 'Na alichukuliwa kama mtu ambaye anavunja torati.' Kwa sababu kile kilichotabiriwa kwa ajili yangu kinatimizwa.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha wakasema, “Bwana, tazama! Hizi hapa panga mbili.” Na akawaambia”yatosha.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Baada ya chakula cha usiku, Yesu aliondoka, kama ambavyo amekuwa akifanya mara kwa mara, akaenda mlima wa Mzeituni, na wanafunzi wakamfuata.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Walipofika, aliwaambia, “Ombeni kwamba msiingie majaribuni.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akaenda mbali na wao kama mrusho wa jiwe, akapiga magoti akaomba,
Square Portrait Landscape 4K UHD
akisema, “Baba, kama unataka, niondolee kikombe hiki. Lakini si kama nitakavyo mimi, lakini mapenzi yako yafanyike.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha malaika kutoka mbinguni akamtokea, akamtia nguvu.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akiwa katika kuugua, akaomba kwa dhati zaidi, na jasho lake likawa kama matone makubwa ya damu yakidondoka chini.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakati alipoamka kutoka katika maombi yake, alikuja kwa wanafunzi, na akawakuta wamelala kwa sababu ya huzuni yao,
Square Portrait Landscape 4K UHD
na akawauliza, “Kwanini mnalala? Amkeni muombe, kwamba msiingie majaribuni.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakati alipokuwa bado akiongea, tazama, kundi kubwa la watu likatokea, na Yuda, mmoja wa mitume kumi na wawili akiwaongoza. Akaja karibu na Yesu ili ambusu,
Square Portrait Landscape 4K UHD
lakini Yesu akamwambia, “Yuda, je unamsaliti Mwana wa Adamu kwa busu?”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakati wale waliokuwa karibu na Yesu walipoona hayo yanayotokea, wakasema, “Bwana, je tuwapige kwa upanga?”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha mmoja wao akampiga mtumishi wa kuhani mkuu, akamkata sikio lake la kulia.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yesu akasema, “hii inatosha. Na akagusa sikio lake, akamponya.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yesu akasema kwa kuhani mkuu, na kwa wakuu wa hekalu, na kwa wazee waliokuja kinyume chake, “Je mnakuja kana kwamba mnakuja kupambana na mnyang'anyi, na marungu na mapanga?
Square Portrait Landscape 4K UHD
Nilipokuwa pamoja nanyi siku zote kwenye hekalu, hamkuweka mikono yenu juu yangu. Lakini hii ni saa yako, na mamlaka ya giza.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakamkamata, wakamuongoza, wakamleta nyumbani mwa kuhani mkuu. Lakini Petro akamfuatilia kwa mbali.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Baada ya kuwa wamewasha moto katika ule uwanda wa ndani na walipokwisha kukaa chini pamoja, Petro akakaa katikati yao.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mtumishi mmoja wa kike akamuona Petro alipokuwa amekaa katika mwanga utokanao na moto, akamtazama akamwambia, “Huyu mtu pia alikuwa pamoja naye.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini Petro akakana, akasema, “mwanamke, mimi simjui.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Baada ya muda kidogo, mtu mwingine akamuona akasema “Wewe pia ni mmoja wao”. Lakini Petro akajibu, “Mwanaume, mimi siyo.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Baada ya kama saa moja hivi, mwanaume mmoja akasisitiza akasema, “Kweli kabisa huyu mtu pia alikuwa pamoja naye, maana ni Mgalilaya.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini Petro akasema, “Mwanaume, sijui usemalo.” Na mara, wakati akiongea, jogoo akawika.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akageuka, Bwana akamtazama Petro. Na Petro akalikumbuka neno la Bwana, pale alipomwambia, “Kabla ya jogoo kuwika leo, utanikana mimi mara tatu.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha wale wanaume waliokuwa wakimlinda Yesu, wakamdhihaki na kumpiga.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Baada ya kumfunika macho, wakamuuliza, wakisema, “Tabiri! Ni nani aliyekupiga?”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakaongea mambo mengine mengi kinyume cha Yesu na kumkufuru yeye.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mara ilipokuwa asubuhi, wazee wa watu walikusanyika pamoja, wakuu wa makuhani na waandishi. Wakampeleka kwenye Baraza,
Square Portrait Landscape 4K UHD
wakisema, “Kama wewe ni Kristo, tuambie.” Lakini yeye akawaambia, “Kama nikiwaambia, hamtaniamini,
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini kuanzia sasa na kuendelea, Mwana wa Adamu atakuwa amekaa mkono wa kuume wa nguvu ya Mungu.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wote wakasema, “Kwa hiyo wewe ni Mwana wa Mungu?” Na Yesu akawaambia, “Ninyi mmesema mimi ndiye.”
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakasema, “Kwa nini bado tunahitaji tena ushahidi? Kwa sababu sisi wenyewe tumesikia kutoka katika kinywa chake mwenyewe.”
Available Bible Translations
Luke 22 (ASV) »
Luke 22 (KJV) »
Luke 22 (GW) »
Luke 22 (BSB) »
Luke 22 (WEB) »
Luc 22 (LSG) »
Lukas 22 (LUTH1912) »
लूका 22 (HINIRV) »
ਲੂਕਾ 22 (PANIRV) »
লূক 22 (BENIRV) »
லூக்கா 22 (TAMIRV) »
लूक 22 (MARIRV) »
లూకా 22 (TELIRV) »
લૂક 22 (GUJIRV) »
ಲೂಕನು 22 (KANIRV) »
لُوقا 22 (AVD) »
הבשורה על־פי לוקס 22 (HEB) »
Lucas 22 (BSL) »
Lu-ca 22 (VIE) »
Lucas 22 (RVA) »
Luca 22 (RIV) »
路 加 福 音 22 (CUVS) »
路 加 福 音 22 (CUVT) »
Luka 22 (ALB) »
Lukas 22 (SV1917) »
Луки 22 (RUSV) »
Луки 22 (UKR) »
Lukács 22 (KAR) »
Лука 22 (BULG) »
ルカによる福音書 22 (JPN) »
Lukas 22 (NORSK) »
Łukasza 22 (POLUBG) »
Luukos 22 (SOM) »
Lukas 22 (NLD) »
Lukas 22 (DA1871) »